Saturday, December 10, 2016

WAHAMIAJI HARAMU 81 WAKAMATWA BAGAMOYO LEO TAREHE 10 DESMBA 2016.


Raia wa Ethiopia  81 wamekamatwa Bagamoyo wakiwa katika katika harakati za  kusafirishwa kupitia  usafiri  wa Baharini.

Akitoa Taarifa  kwa waandishi  wa Habari  mkuu  wa wilaya ya  Bagamoyo,  Alhaji, Majid Mwanga, alisema watu hao  wamekamatwa kufuatia  ushirikiano na raia wema  ambao  walitoa taarifa  polisi  na kufanikisha  kuwakamata  watu hao  ambao  wameingia nchini bila ya  kufuata sheria.

Alisema  tukio hilo limetokea  leo Tarehe  10  Desemba,  kitongoji  cha    Mjimpya kata ya  Kisutu katika eneo la kingani ambapo watu hao walikutwa hapo.

Alisema vyombo vya ulinzi  wilayani  Bagamoyo vimejipanga kukomesha  vitendo vyote  vya  kihalifu ikiwa ni  pamoj a upitishaji  wa biashara za  magendo na  wahamiaji  haramu.

Aidha,  aliwataka wananchi  kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na Usalama  ili kufichua  maovu  mbalimbali yanayofanyika katika wilaya ya  Bagamoyo.

Akizungumzia  madhara ya  kuwaficha  wahamiaji haramu  ni  pamoja  na kukithiri kwa vitendo vya  kihalifu na kuambukizana  magonjwa kutokana na  kuwa waliongia bilaya   vibali hawakupitia kwenye ngazi za kuwahakiki ikiwa wana  magonjwa ya  kuambukiza au  la.
 
Mmoja wa  wahamiaji hao Shemsadin Wesorow, akizungumza kwa niaba ya  wenzake alisema  wametokea katika  Nchi ya Ethiopia  lengo  likiwa ni  kwenda  Afrika ya  Kusini  kufanya  kazi na kwamba hawakutoroka kutoka  kwao.

Alisema  alipigiwa simu  na  kaka yake ambae anamiliki Duka  kubwa huko  Afrika ya  kusini  ili aende  nae  akapate  kazi.

Akizungumzia ni kwa namna gani  wangeweza kuishi  huko hali ya wako  wengi,  Shemsadini  alisema kila mmoja kati yao ana ndugu  huko kwahiyo isingekuwa tabu  kuishi huko.

Alipoulizwa kuhusu idadi kamili  katika msafara wao alisema  wametoka 93 lakini waliokamatwa na  polisi ni 81 tu na 12 waliobaki wamekimbilia vichakani.

Aidha, ameiomba  serikali ya Tanzania iwasaidie  kurudi  nchini kwao  na kwani baadhi yao wamechoka kwa njaa huku wengine  wakiwa wanaumwa bila ya kupata matibabu  kutokana  na  mazingira ya kujificha  katika safari yao.





Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid  Mwanga.

No comments:

Post a Comment