Friday, December 16, 2016

WAZIRI JENISTA MHAGAMA ATEM BELEA UJENZI WA SOKO LA NAFAKA KATA YA MAGOMENI BAGAMOYO.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na watu wenye Ulemavu, Mh. Jensta Mhagama kulia, akipokea Taarifa ya ujenzi wa soko la nafaka lililopo Kitongoji cha Maji coast, kata ya Magomeni, Bagamoyo mjini, katikati ni Mhandisi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Henrico Shauri, na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Najid Mwanga.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira  na watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama amemuagiza Mhandisi wa Halmashuri ya Bagamoyo, Henrico Shauri, kukamilisha  kazi zilizobaki ndani ya wiki mbili ili Soko hilo liweze kufunguliwa mwezi January 2017.

Waziri Jenista Mhagama alitoa agizo hilo  alipotembelea  ujenzi wa soko hilo  ambapo ameridhishwa na shughuli za ujenzi zilivyoenda na kusema kuwa hakuna sababu ya kuchelewa kulifungua soko hilo ili wananchi waweze kufaidika na uwepo wa soko hilo.

Alisema mpaka kufikia Tarehe 30 mwezi Desemba kila kitu kiwe kimekamilika ili mwezi January  liweze kufunguliwa, ambapo waziri mkuu anatarajiwa kulifungua soko  hilo.








No comments:

Post a Comment