Monday, December 5, 2016

VIKUNDI VYA KINAMAMA NA VIJANA BAGAMOYO VYAFAIDIKA NA ASILIMIA 10 ZA HALMASHAURI.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, akikabidhi Hundi ya shilingi Milioni  3 kwa kikundi cha  Jipe moyo kilichopo  kijiji  cha  Hondogo Halmashauri ya Chalinze.
Mkuu wa wilaya ya  Bagamoyo, Majid  Mwanga  akikabidhi  Hundi ya shilingi milioni  2 kwa kikundi cha  Umoja ni  Nguvu kilichopo kijiji cha  Lupungwi.
.....................................
Halmashauri ya Chalinze imegawa  fedha za kina mama na vijana ili kujiendeleza katika shughuli  mbalimbali za kiuchumi.

Akizungumza  kabla kukabidhi hundi kwa  vikundi vya Jipe Moyo na Umoja ni nguvu, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga  alisema vikundi vyote vilivyopata fedha hizo vinapaswa kuziingiza kwenye  miradi mbalimbali ili wazirejeshe kwaajili ya kuendelea na mgao kwa vikundi vingine.

Alisema fedha hizo zimetokana na asilimia10 inayotengwa katika Halmashauri kwaajili  kina mama na vijana ambapo Halmashauri ya Bagamoyo imetenga shilingi milioni 126 na Halmashauri ya Chalinze imetenga milioni 79.

Aidha, mkuu huyo wa wilaya aliwasifu wakurugenzi wa Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze kwa  kusimamia vyema mapato na kuwapongeza madiwani  kwa  kusimamia asilimia kumi kwaajili ya kina mama na vijana.

Katika mgao huo kikundi cha Jipe moyo kutoka kijiji cha Hondogo, kimepata shilingi milioni 3 na kikundi cha  Umoja ni Nguvu kutoka kijiji cha Lupungwi kimepata milioni 2.


No comments:

Post a Comment