Saturday, December 10, 2016

09 DESEMA, DC. BAGAMOYO AZINDUA KILIMO CHAMA CHA USHIRIKA RUVU (CHAURU)


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaji, Majid Hemed Mwanga, leo Tarehe 09 Desemba 2016 amezindua rasmi kilimo katika shamba  la Chama cha Ushirika Ruvu, (CHAURU) kwa msimu wakilimo kwa mwaka 2016/17.

Akizungumza wakati wa uzinduzi  huo, mkuu huyo wa wilaya aliwataka CHAURU kuanzisha utaratibu wa kuuza mchele badala ya mpunga ili kupata soko kwa urahisi na kupunguza mfumuko wa bei ya Mchele katika Halmashauri ya Chalinze.

Alisema kutokana na uchaguzi mzuri wa mbegu inayotum ika katika mashamba hayo, mchele unaolimwa CHAURU umekuwa mzuri na kwamba unao uwezo wa kuingizwa kwenye ushindani  wa  kibiashara.
 Mkuu wa wilaya ya  Bagamoyo, Majid  Mwanga, akizungumza katika Mashamba ya  Chama cha Ushirika Ruvu (CHAURU)
 Baadhi ya Matrekta yaliyokuwa yakizindua kilimo katika Mashamba ya CHAURU.

No comments:

Post a Comment