Tuesday, December 6, 2016

UFAFANUZI KUHUSU MIZIGO YA WAMA BANDARINI.

index 
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuutaarifu umma kuwa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) iliingiza nchini maboksi kumi na moja (11) ya vitabu/kamusi kutoka nchini Japani kwa ajili ya matumizi ya elimu.

Kwa mujibu wa sheria ya forodha ya Afrika Mashariki (The East African Community Customs Management Act, 2004), pamoja na Sheria ya Ongezeko la Thamani (VAT Act, 2015), vitabu hivi havitozwi kodi ya forodha wala ya Ongezeko la Thamani (VAT).

Vitabu hivi vililipishwa tozo ya uondoshaji mizigo bandarini (Customs Processing fees) shilingi 42,483 na tozo ya Maendeleo ya Reli (Railway Development Levy) shilingi 106,438 ikiwa ni jumla ya shilingi 148,921. Baada ya malipo hayo kufanyika, vitabu hivyo vilichukuliwa na WAMA tangu tarehe 10 , 2016.

Tunapenda kutoa ufafanuzi kwamba taarifa zilizoandikwa na baadhi ya magazeti hivi karibuni juu ya vitabu hivyo kuwamo katika orodha ya bidhaa zinazopaswa kupigwa mnada kwa sababu ya kutolipiwa kodi siyo sahihi.

Kwa kuwa vitabu hivyo havikupaswa kulipiwa kodi ya Forodha wala VAT kwa mujibu wa sheria, ni wazi kuwa WAMA hawakupaswa kuomba msamaha wa kodi kwenye Mamlaka yoyote ile.  

Orodha iliyowahi kuchapishwa na baadhi ya magazeti hapa nchini na ambayo ilijumuisha jina la WAMA haikuwa sahihi.
Pamoja Tunajenga Taifa Letu
1.   J. Kidata
KAMISHNA MKUU

No comments:

Post a Comment