Saturday, December 10, 2016

MZEE WA BARAZA KIBAHA, AHUKUMIWA JELA MIAKA 3 KWA RUSHWA.

Mahakama ya hakimu mkazi kibaha, imemuhukumu mzee wa baraza Francis Issaya (64) kwenda jela miaka 3 au kulipa faini laki 5 baada ya kukutwa na hatia ya kupokea Rushwa.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Harieth Mwailolo amesema mahakama hiyo imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa jamuhuri na hivyo anatoa adhabu ya kwenda jela kwa mzee huyo ili iwe fundisho kwa wengine. 

Awali mwendesha mashitaka wa Takukuru Sabina Weston aliieleza mahakama hiyo kuwa mzee huyo wa baraza alitenda kosa hilo mwezi uliopita kwa kumshawishi Omari Hiza ampe kiasi cha Tshs. 100,000/= ili aweze kumsaidia mkewe Mariam Hussein aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya Jinai 329/2016 kosa Shambulio la kudhuru mwili.

Wakati huohuo Mahakama ya hakimu mkazi kibaha ya mhukumu Abduly Omar (27) mkazi wa kwa mathias kibaha kwenda jela miaka 30 baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kujaribu kubaka. 

Akisoma hukumu hiyo hakimu mkazi wa mahakama ya hakimu mkazi kibaha Aziza Mbadyo alieleza kuwa mahakama imeridhika na ushahidi uliowasilishwa kwenye mahakama hiyo usio acha shaka yoyote hivyo mtuhumiwa ataenda jela miaka hiyo ili iwe fundisho kwa wengine. 

Awali mwendesha mashitaka wa serikali Lulu Ukwaju aliileza mahakama hiyo kuwa mnamo tarehe 07 July 2016 huko kwa Mathias Kibaha Abduly Omary alijaribu kumbaka binti ambaye jina linahifadhiwa kwa sasa na kabla ya kutekeleza azima yake hiyo alikurupushwa na wanachi

No comments:

Post a Comment