Friday, September 29, 2023

CHATANDA AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM WILAYANI CHATO. 

 


Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT, Mary Chatanda, amefurahishwa na Utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani Chato Mkoani Geita alipotembelea Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika wilaya hiyo .

Akizungumza leo  katika Mradi  wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato Mwenyekiti Chatanda amewapongeza viongozi wa Serikali chini ya Mkuu wa wilaya ya Chato Deusdedith Katwale ambaye ameshirikia na Mkurugenzi wake wa Halmashauri kwa usimamizi na Ufanisi wa hali ya Juu .

" Fedha ya Serikali zaidi ya Bilion 31 imejenga Hospitali hii ya Kanda ya Chato niwaombe wauguzi wa Hospitali hii muwahudumie wagonjwa vinzuri kwa kuwa wananchi mbalimbali watakuja kutibiwa hapa hivyo Uadilifu, upendo na hekima ili wananchi wafurahie matunda ya Rais Samia kwa upande wa  afya katika kupata huduma bora kwa wauguzi wao."

 

No comments:

Post a Comment