Friday, September 29, 2023

CP. WAKULYAMBA ATOA SOMO LA MIONGOZO YA JESHI LA UHIFADHI.

 

Na Sixmund Begashe


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Kamishna Benedict Wakulyamba amewataka askari wa Jeshi la Uhifadhi kufanya kazi kwa kufuata Miongozo, Kanuni na kuzingatia sheria zilizopo ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Uhifadhi.

CP. Wakulyamba ametoa kauli hiyo Jijini Arusha kwenye Warsha maalum aliyoianda kwa Maafisa wa Jeshi la Uhifadhi chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kukumbushana masuala mbalimbali ya uhifadhi pamoja na haki za binadamu kama sehemu ya utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan la kumtaka arejeshe nidhamu ya Jeshi hilo.


Katika somo alilotoa kwa Maafisa hao wa Jeshi la Uhifadhi, CP. Wakulyamba alisisitiza nidhamu katika matumizi sahihi ya sare za Jeshi hilo pamoja na matumizi ya nguvu katika kukabiliana na uhalifu hususani kwenye matumizi ya Silaha.



Aidha CP. Wakulyamba amelitaka Jeshi hilo kuimarisha mahusiano mema na Vyombo vingine vya ulinzi na Usalama, taasisi za Serikali na wananchi kwa ujumla kuwa kazi ya uhifadhi ni jukumu la kila Mtanzania kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kinachokuja.












No comments:

Post a Comment