Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Boniventure Mushongi.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Makachero wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani wakishirikiana na wale kutoka Makao Makuu ya Polisi, tunamshikilia Khalid Mohamed (29) ambae ni fundi ujenzi na mkazi wa kwa Mathias Wilaya ya Kibaha akiwa na Silaha aina ya SMG na risasi 14.
Mtuhumiwa huyo, tulimkamata huko eneo la
Misugusugu Kata ya Misugusugu na Tarafa na Wilaya ya Kibaha akiwa na Silaha hiyo aina ya SMG
ambayo namba zake zimefutwa pamoja na risasi 14
jana Tarehe 02/03/2017 majira ya 17:15
HRS.
Mtuhumiwa huyo,
mb ali na kukutwa na Silaha hiyo,
pia alikutwana risasi 4 za Shotgun, Mlipuko mmoja, Sime moja, maski moja na koti moja vyote vikiwa
vimehifadhiwa kwenye mfuko wa Rambo chini ya Ardhi kwenye Shamba la mtu aliyejulikana kwa jina moja
la Swai.
Uchunguzi
wa Awali umeweza kubaini kuwa, mtuhumiwahuyo na wenzake wengine 15 ambao
tunawashikilia wamekiri kujihusisha na matukio ya uporaji kwenye maeneo mbalimbali
ya Mkoa wa Pwani, likiwemo
tukio la mauaji ya aliyekuwa Mkuu
wa Wilaya ya Liwale mwaka
2012-2016, Ephraim Mfingi
Mbaga (54) aliyuwawa akiwa nyum
bani kwake baada ya kupigwa risasi
kwenye paja lamguu wa
kushoto na kujeruhiwa kwa kitu
chenye ncha kali ambapo alipoteza maisha
akiwa njiani akipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi.
Imetolewa na:-
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani
Boniventure Mushongi (ACP)
03 March 2017.
No comments:
Post a Comment