Friday, May 31, 2024

DED BAGAMOYO AFUNGUA MAFUNZO KUHUSU MABORESHO YA MITAALA YA ELIMU YA AWALI, MSINGI, SEKONDARI NA UALIMU KATIKA SHULE YA SEKONDARI BAGAMOYO MKOANI PWANI.

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw Shauri Selenda tarehe 30 Mei 2024 amefungua mafunzo kuhusu maboresho ya mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari katika Shule ya Sekondari ya Bagamoyo Mkoani Pwani.


Mafunzo hayo, yamelenga kuwapitisha washiriki katika muundo wa Elimu, Maboresho Elimu Msingi na Sekondari pamoja na Ualimu.


" Ndugu zangu nyinyi mliopo hapa ni asilimia ndogo sana ya washiriki wanaohitajika kupata mafunzo haya, hivyo nawaomba muwe makini kutumia muda Ili muweze kupata Yale yaliyotarajiwa kutoka kwa wawezeshaji wetu ". Alisema Bw Selenda.


Mafunzo haya ya siku mbili yanajumuisha Walimu Wakuu 78 toka Shule za Msingi za Serikali na binafsi Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo. Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Ofisi ya Raisi- TAMISEMI






No comments:

Post a Comment