Saturday, May 11, 2024

RUNALI WAGAWA VITENDEA KAZI KWA WAKULIMA KUELEKEA MSIMU WA UFUTA NA MBAAZI

 

CHAMA kikuu cha ushirika (RUNALI) kinachounganisha wakulima wa Wilaya za Ruangwa,  Nachingwea na Liwale Mkoani Lindi kimegawa jumla ya viroba laki 800,000, vitabu pamoja na kamba kwa wakulima wa wilaya ya Nachingwea, Ruangwa na Liwale kuelekea msimu wa mauzo ya mazao ya ufuta,Mbazi na Korosho.


 uzinduzi wa ugawaji wa vifungashio hivyo ulioenda sambamba na utoaji wa mafunzo wa matumizi mfumo wa TMX kwa watendaji wakuu wa vyama vya msingi (AMCOS) yaliyofanyika huko Wilayani Nachingwea.


Akizungumza wakati wa zoezi hilo meneja wa chama hicho Jahida Hassan alisema kuwa wamegawa vifungashio hivyo kwa lengo la kuwawezesha wakulima kuhifadhi mazao kwenye ubora unaotakiwa sokoni.


Bi. Jahida  alisema kuwa RUNALI wamekuwa wanatoa elimu mara kwa mara kwa wakulima ili waweze kulima kilimo kilicho bora na kufanikiwa kupeleka mazao yaliyo bora sokoni.


" tupo  tayari kwa kuanza msimu mpya wa Mbaazi na ufuta na lengo la mafunzo haya ni kuwajengea utayari wa kwenda kwenye msimu mpya pia wametoka kufahamishana umuhimu wa kufanya ukaguzi.


  mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Adinan Mpyagila amewasihi wakulima kutouza mazao kiholela na kuweka vituo kwenye mipaka ya wilaya ili mazao yasiuzwe nje ya wilaya kwa kuwa itapelekea kupoteza mapato ya Halmashauri kwenye mazao ya mbaazi na ufuta.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha ushirika (RUNALI) Odas Mpunga amewapongeza vyama vya Ushirika kwa kazi kubwa waliyofanya na kuingiza mapato makubwa. Pia, amewataka kuyatumia vyema mafunzo haya kwa vitendo ili kuleta Matokeo chanya.






No comments:

Post a Comment