Tuesday, May 14, 2024

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 40 MTAMA KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA

 

Na HADIJA OMARY 

LINDI.

Zaidi ya wananchi Elfu 40 kutoka katika Halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi wanatarajiwa kunufaika na mradi wa Maji na usafi wa mazingira unaotekelezwa  na taasisi isiyo ya kiserikali ya 'Heart to Heart' chini ya ufadhili wa Shirika la Kimataifa la KOICA utakaogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 1.6

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo katibu tawala Mkoa wa Lindi Bi zuwena Omary amewahimiza wananchi na taasisi mbalimbali zilizopo ndani ya Mkoa huo kutunza na kulinda vyanzo vya maji ili viendelee kutoa maji kwa muda mrefu. 

amesema upatikanaji wa maji safi na ya uhakika unategemea na utunzaji wa mazingira kuzunguka vyanzo vya maji  ikiwemo upandaji miti huku pia akitaka kamati za maji na mazingira zishirikishwe ili kufikia malengo ya mradi huo.

Mratibu wa mradi kutoka Heart to Heart Innocent Deus  amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa miaka sita kwa awamu tofauti ambapo kwa awamu ya kwanza utatekelezwa kwa miaka mitatu katika halmashauri ya Mtama na kuvifikia vijiji 87, na kaya zaidi ya elfu 40.


Amesema  Mradi huo una dhumuni la kupeleka huduma ya maji kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kuhakikisha usafi wa mazingira unazingatiwa kuanzia ngazi ya vijiji hadi Wilaya.

Kwa upande wake Ismail Mbani Afisa afya na  mazingira Halmashauri ya Mtama amesema Mradi  huo wa maji  utasaidia kuboresha upatikanaji wa huduma hiyo na kuboresha usafi wa mazingira kwa Wananchi.

"Mradi huo utawasaidia hasa katika swala la uboreshaji wa vyoo ambapo kwa sasa hali ya vyoo katika halmashauri hiyo ni asilimia 54% ambapo hata hivyo kutokana na mvua zilizonyesha zilipelekea asilimia 1.7 ya kaya katika halmashauri hiyo kukosa vyoo kabisa hivyo basi kupitia mradi huu kutakuwa na maboresho makubwa katika eneo hii"





No comments:

Post a Comment