Saturday, May 25, 2024

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AKOSHWA NA MRADI WA KITEGA UCHUMI WILAYA YA LIWALE 

 

KIONGOZI wa Mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2024 Godfrey Mzava  ameonyesha kuridhishwa na mradi wa  ujenzi wa vibanda 34 vya biashara katika eneo la stendi kuu ya mabasi Halmashauri ya wilaya ya Liwale  wenye Thamani ya shilingi milioni 137, 754, 450.00

Akizungumza mara baada ya kutembelea na kuona utekelezaji wa mradi Mzava ameipongeza halmashauri hiyo kwa maono makubwa ya kuongeza chanzo kipya cha mapato  kitakachowasaidia katika shughuli mbalimbali za maendeleo 

Hata hivyo Mzava ametoa siku tatu kwa halmashauri hiyo kuandaa mikataba mipya watakayoingia na wafanyabiashara wanaotumia vibanda hivyo

" pamoja na kuwapongeza kwa kubuni chanzo cha mapato lakimi niwaagize halmashauri kuandaa mikataba mipya mutakayowapa wafanyabiashara hawa ambao wapo kwenye vibanda hivi ndani ya siku tatu kuanzia leo mei 25 hadi 29 mwenge wa uhuru uwe umeshapata taarifa ya utekelezaji wake" alisisitiza Mzava

Kwa upande wake kaimu afisa Mipango wa halmashauri hiyo Hamisi Abdallah  amesema Ujenzi wa vibanda hivyo ulilenga kuongeza vyanzo vipya katika halmashauri hiyo  ambapo hadi sasa halmashauri imeshakusanya shilingi milioni 25, 296,500.00 zilizotokana na ukodishaji wa vibanda hivyo kati ya bajeti ya shilingi 44, 480, 000.00 zilizopangwa kukusanywa kwa mwaka 2023/2024

" kukamilika kwa mradi huu, umewezesha  mazingira mazuri ya wananchi kujiajiri wenyewe na pia kuongeza wigo wa ukusanyaji wa  mapato ya Halmashauri na kodi kwa TRA"

Kwa upande wake   Johari Hamisi mfanyabiashara katika vibanda hivyo amesema toka halmashauri kujenga vibanda hivyo ha wao kukodishwa wamekuwa wakinufaika kutokana na kuwa na  mazingira mazuri na ya kuvutia ya kufanyia biashara 







No comments:

Post a Comment