Saturday, June 1, 2024

NMB YATOA MSAADA VIFAA TIBA VYA MILIONI 10 HOSPITALI YA BAGAMOYO

 

Benki ya NMB yatoa msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo ikiwa ni kutekeleza majukumu yao ya kusaidia wananchi katika kuimarisha afya zao.


Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Meneja wa kanda ya Dar es salaam, Ferdinand Mpona, amesema NMB imetekeleza msaada huo ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali chini ya uongozi wake Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda, amesema wanaishukuru Benki ya NMB kwa kutoa vifaa hivyo kwani vitasaidia katika matibabu ya afya za wananchi.


Amesema serikali imetenga fedha za kujenga na kukarabati majengo mbalimbali ya Hospitali ya Bagamoyo hivyo inapokea taasisi binafsi zikajitolea kusaidia vifaatiba inasaidia kuongeza ufanisi katika kuwahudumia wananchi.


Vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na Vitanda vitano vya kujifungulia kinamama wajawazito, pamoja na magodoro yake, na viti vya magurudumu (wheelchairs) ishirini kwaajili ya kubebea wagonjwa ambavyo vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 10.







No comments:

Post a Comment