Wednesday, May 8, 2024

MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA WAFIKA LINIDI

 


Na Mwandishi wetu

Lindi

Zaidi ya Madaktari 50 ambao ni Bingwa na Wabobezi wa Rais Samia Suluhu  wameweka kambi maalumu ya matibabu ya Afya katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Lindi Sokoine kwa siku 5 kuanzia tarehe 6 mai hadi 10.

Akizindua utoaji wa  matibabu hayo mkuu wa wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Lindi  amesema huduma hizo za kibingwa zitarahisisha kwa kiasi kikubwa huduma kwa kuwafikia wananchi na hivyo kupunguza gharama ya kusafiri kwenda nje ya mkoa huo kufuata huduma hizo.

'Tunatoa shukrani za dhati kwa Rais wetu Dkt samia kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya utoaji wa huduma za Afya kwa kuhakikisha anapeleka fedha za ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za Afya pamoja na manunuzi ya vifaa tiba” alisema Ndemanga

Aidha, Ndemanga amewaomba Wananchi wote wenye matatizo ya kiafya kuhudhuria katika kambi hiyo ili kuonana na kutibiwa na Madaktari Bingwa na Bingwa bobezi ambapo itasaidia kuwapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu nje ya mkoa kufuata huduma.

Dkt.Alexander Makalla ambaye ni mganga mfawidhi wa hospitali ya Rufaa Sokoine amesema ili kuwafikia wananchi wengi zaidi huduma za kumuona daktari zitatolewa bure isipokiwa kwa wagongwa waliokuwa na Bima za Afya huku mgonjwa akitakiwa asilimia 70 kwa huduma za vipimo, upasuaji na dawa.

Amesema huduma zitakazotolewa ni pamoja na Magonjwa ya wanawake na uzazi, Magonjwa ya Watoto, Magonjwa ya mfumo wa mkojo, magonjwa ya ngozi, Magonjwa ya kinywa na meno.

Huduma zingine ni Magonjwa ya macho, Magonjwa ya Afya ya akili pamoja na magonjwa ya pua, koo na Masikio pia huduma za mazoezi Tiba na viungo, upimaji wa saratani ya mlango wa kizazi na matiti pamoja na huduma za vipimo vya maabara, mionzi na upasuaji

Naye Meneja wa mfuko wa taifa wa bima ya afya Irine Katarahiya ametumia fursa hiyo kuwahasa wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili waweze kunufaika na huduma lukuki.

" Kwa Mkoa wa Lindi hii ni fursa hasa kwa wale wenye kadi ya mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  kwa sababu kadi yake inamuwezesha kumuona daktari yeyote Madaktari zaidi ya  hamsini wako hapa Mkoani Lindi hivyo nitumie fursa hii kuwahasa wananchi amabo bado hawajakata kadi za Bima za Afya kufanya hivyo ili kuweza kunufaika na fursa zijazo"Alisema

Nao baadhi ya wananchi waliofika kupata matibabu hayo wakamshukuru Rais Samia kwa kuwasogezea huma hizo karibu yao.



No comments:

Post a Comment