Wednesday, November 30, 2016

MAADHIMISHO YA SIKU YA WALEMAVU KITAIFA YAFUTWA

index
Maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani, ambayo kitaifa yalitarajiwa kufanyika jijini Dar es salaam,Desemba 3, mwaka huu yameahirishwa na badala yake kila mkoa utaadhimisha kivyake.

Akitoa tamko la kuharishwa kwa maadhimisho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), George Simbachawene amesema maadhimisho hayo yalilenga kila halmashauri isafirishe wanachama wa vyama vya watu wenye ulemavu ili washiriki maadhimisho hayo jijini humo.

Amesema kwa mujibu wa maelekezo aliyopewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa wakuu wa mikoa kuwa badala ya maadhimisho hayo ya kitaifa kukusanya walemavu wote kwenye mikoa kwenda Dar es salaam yafanyike kwenye mikoa yao.

No comments:

Post a Comment