Monday, November 28, 2016

BONANZA LA MICHEZO BAGAMOYO, HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAICHAPA KILUNGULE MABAO 3-0.

Bonanza  la michezo liliofanyika jana Tarehe 27 Novemba, katika uwanja wa Mwanakalenge Bagamoyo mjini, limejumuisha timu 11 kutoka Dar es slaam na  Pwani na kulifanya  liwe kivutio cha aina yake  pale timu za maveterani zilipomenyana vikali katika kuonyeshana  uwezo.

Katika michezo hiyo timu ya Halmashauri ya Bagamoyo iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya timu ya Kilungule, Timu ya  Mapinga ilichuana na Neibour ambapo Neibour ilitoka na ushindi wa bao 1 na Mapinga haikupata kitu.

Aidha katika Mechi nyingine Mapinga ilicheza na Temboni ambapo Temboni  waliichapa Mapinga bao  1-0,  Timu ya Mwenge Veterani imeilaza Timu ya Leaders mabao 2-0, huku Corner ikwa imeichapa Kibamba mabao 2-0, na Kibaoni imeibuka na ushindi wa bao 1 dhidi ya Golan ambayo haikupata kitu.

Kwa upande wake Mratibu wa Bonanza hilo, Deodatus Katambi alisema Bonanza hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa  kwakuwa   matarajio yalikuwa ni kuwa na timu 6 lakini zimepatikana timu 11 zilizoshiriki katika michezo hiyo.

Alisema watu wanapenda Michezo bila ya  kujali umri wao na kwamba kinachokosekana ni kumpata mtu wa kuwaunganisha  pamoja ili waweze kuonyesha uwezo wao.

Katambi ambae ni katibu wa Temboni Veterani ambao ndio walioandaa Bonanza hilo, alisema timu zote zilionyesha uwezo mzuri na kupelekea ushindani kuwa mkubwa jambo ambalo liliwavutia watazamaji.

Aliongeza kwa kusema kuwa, timu ya Halmashauri ya Bagamoyo ilikuwa vizuri katika mchezo na kutoa wito kwa serikali kuzijengea uwezo timu za Halmashauri ili kupata timu bora itakayoleta burudani katika sherehe  mbalimbali na kuwajengea afya bora kutokana na mazoezi.

Mechi hizo zilizochezwa katika uwanja wa mwanakalenge mjini Bagamoyo zilichezeshwa na waamuzi Raphael Ntasi, Idi  Mpingo, Jafari Shaweji, wengine ni Hamadi  Kidodi, Shabani  Milao na Mohamedi  Toloa. 
Wachezaji wa timu ya Temboni veterani wakiwa katika Picha ya Pamoja kabla ya pambano lao na Mapinga Veterani, katika  Bonanza  la michezo lililofanyika uwanja wa Mwanakalenge Bagamoyo mjini.
Nyama choma, vinywaji na  vyakula vilipatikana katika Bonanza hilo 
 Wachezaji pamoja na watazamaji wakiwa wametulia kufuatilia michezo iliyokuwa ikiendelea
Mratibu m kuu wa Bonanza hilo kutoka Tembeni Veterani, Deodatus Katambi akizungumza na waandishi wa Habari. 

No comments:

Post a Comment