Monday, November 28, 2016

MAHAFALI SEKONDARI YA YEMEN, WAHITIMU WATAKIWA KUWEKA MALENGO YA KUENDELEA NA MASOMO.

Wahitimu wa kidato cha 4 Shule ya Sekondari Yemen iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi Mkurugenzi wa Benki ya Amana, Dkt. Muhsin Masoud akizungumza katika mahafali hayo.
.............................
 
Vijana waliomaliza elimu ya sekondari  wametakiwa kuweka malengo ya kuendelea na elimu ya juu ili  kuongeza ufahamu  wa mambo mbalimbali katika maisha yao.

Wito huo umetolewa na mkurugenzi wa Benki ya Amana, Dkt. Muhsin  Masoud alipokuwa akizungumza katika mahafali ya wahitimu wa kidato cha nne katika shule Sekondari yemen iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Dkt. Muhsin  ambae alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo, amesema Kidato cha nne sio mwisho wa  elimu na kwamba kila muhitimu anatakiwa kujiwekea malengo ya kuendelea na elimu ya  juu.

Aliongeza kwa kusema kuwa, sio lazima ukimaliza kusoma ukaajiriwe bali elimu itakufanya uweze hata  kuendesha mambo yako kwa ufanisi.

Aidha, aliwataka   vijana  wahitimu  kuwa waadilifu  katika shughulizao mbalimbali katika jamii kwani tabia hiyo ya uadilifu  itawajengea heshima na  uaminifu.

Kwa  upande wake Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Astahili Akilimali, amewataka wazazi na walezi kuendelea kuwasimamia wahitimu hao  ili wadumishe tabia ya  usomaji wa Qur ani kama walivyokuwa shuleni na kuongeza kuwa hali hiyo itaendelea kuwajengea hofu juu ya Muumba wao.

Aliongeza kwa kuwataka wazazi na  walezi ambao bado wana watoto wao  shuleni hapokutoa ushirikiano na walimu ili kufanikisha malezi ya  wa toto katika kuwapatia elimu.

Alisema haipendezi kwa mzazi  kukaa kimiya bila ya  kuuliza maendeleo ya mwanae kwa mwalimu na kusema kuwa hali hiyo itapelekea mtoto afanye anachotaka kwakuwa hakuna wa kumfuatilia mambo yake.

Nao wahitimu wa kidato cha nne katika shule hiyo ya Yemen  wamesema kuwa wamefurahi  kumaliza kidato cha nne katika shule hiyo na kwamba wamejifunza mambo mbalimbali yakiwemo yanayohusu dini yao.

Aidha, wahitimu hao wameahidi kuendeleza tabia njema walizopata shuleni hapo ili wawe  mfanowa  kuigwa katika jamii.
Meneja wa Shule za Yemen, Jamila Awadh, akizungumza katika mahafali hayo.

Wahitimu wasichana wa kidato  cha 4 Sekondari ya Yemen wakiwa katika mahafali.
Kutoka  kushoto ni  Meneja wa shule za  Yemen, Jamila Awadh, wa  pili kushoto ni mkuu wa shule ya Awali, Sheikha Saad na wa kwanza kulia ni  Afsa rasilimali watu, Anaf Saleh  Karama.
Kutoka kushoto ni  Mgeni rasmi, Dkt. Muhsin Masoud, wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule za Yemen Hassan Akrabi na wa mwisho kulia ni kiongozi  wa wazazi wa shule ya Sekondari Yemen, Abdulazizi Hassan.
Mgeni Rasmi, Dkt. Muhsin Masoud akifuatilia mahafali hayo.
Mwalimu mkuu wa shuleya Sekondari ya Yemen Astahili Akilimali akizungumza  katika Mahafali hayo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya shule za Yemen Hassan Akrabi akizungumza katikaMahafali hayo.
Wazazi na walezi wakichukua picha za matukio kupitia simu zao za mkononi.

No comments:

Post a Comment