Mkuu wa mkoa wa Pwani Mh. Mhandisi Everist
Ndikilo akizungumza na waandishi wa habari shule ya msingi Kibindu katika
Halmashauri ya Chalinze, wilayani Bagamoyo, kushoto ni mkuu wa wilaya ya
Bagamoyo, Mh. Alhaji, Majid Mwanga.
...........................................
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Everist Ndikilo, amempongeza mkuuwa wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga kwa kutembelea maeneo
yake na kubaini changamoto mbalimbali.
Mkuu huyo wa mkoa ameyasema hayo hivi karibuni alipotembelea
kata ya Kibindu wilayani Bagamoyo ambapo alikuta ujenzi wa madarasa ukiendelea huku ukiongozwa na
mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga.
Aidha, amewataka viongozi wote wa serikali mkoani
Pwani kuacha kukaa ofisini pekee na badala yake watembelee maeneo yao ili
kujionea changamoto zilizopo kwenye maeneo mbalimbali na kuzitafutia ufumbuzi.
Alisema kitendo cha mkuu wa wilaya ya Bagamoyo kutembelea maeneo
yake kimepelekea kubaini changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa vyumba vya
madarasa katika baadhiya shule nahivyo ameweza kuchukua hatua ya kuona namna
gani changamoto hiyo inaweza kutatuliwa.
Alimpongeza pia Diwani wa kata ya Kibindu, Mkufya
Ramadhani Mawazo, Mwenyekiti wa kijijicha Kibindu, Yusuf Mahimbo na Afisa
Mtendaji kata ya Kibindu, Godwin Mhagama kwa kushirikiana vyema katika kuwahamasisha
wananchi kushiriki ujenzi wa huo wa madarasa.
Akizungumzia hali hiyo, mwenyekiti wa kijiji cha
Kibindu, alisema wamefanikiwa kwa kuwashirikisha wananchi kila hatua hali
ilyopelekea wananchi kujitokeza kwa wingi katika shughuli hiyo.
Alisema wameweka utaratibu wa
kila siku wanapatikana wananchi wa kitongoji kimoja ili kushiriki shughuli hiyo ya
maendeleo ambapo hiyo inatoa nafasi kwa vitongoji vingine kujiandaa kwaajili ya
siku yao.
Akielezea hali hiyo, mkuu wa wilaya ya Bagamoyo,
Majid Mwanga, alisema amefikia uamuzi wa kuweka kambi katika shule hiyo ili
kufanikisha ujenzi wa vyumba vya madarasa,
ambapo inaupungufu wa vyumba
vyamadarasa.
Alisema tatizo
la madawati katika shule za wilaya ya Bagamoyo limekwisha
na kwamb a kilichobaki sasa ni
kuongeza idadi ya vyumba vya madarasa
katika baadhi ya shule na kuanzisha shule mpya katika maeneo ambayo hakuna
shule ili kuwaondolea watoto adha ya kutembea umb ali mrefu kufuata shule hali
inayopelekea kuchoka.
Akiilezea shule ya msingi Kibindu alisema, shule
hiyo ina wototo zaidi ya elfu moja wakati vyumba vya madarasa ni vinne tu
ambapo watoto hulazimika kukaa chini kwa sababu ya hakuna nafasi ya kuweka madawati.
Aliongeza kwa kuwataka wadau mbalimbali kusaidia
ujenzi wa vyumba vya madarasa katika maeneo yenye mahitaji ili kuisadia
serikali katika kutatua baadhi ya changamoto zilizopo katika jamiii.
Wananchi mbalimbali walioongea na bagamoyokwanza
blog. walisema wamefarijika na kitendo cha mkuu wa wilaya ya Bagamoyo kukaa na
wao kwa
muda wa siku nne huku akishiriki kazi za ujenzi kama mwananchi wa
kawaida.
Walisema hawajawi kuona mkuu wa wilaya kufika
katika kijiji hicho na kukaa nae hivyo kitendo cha mkuu wa wilaya wa sasa Majid
Mwanga ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wengine katika kuwa karibu na
wananchiili kujua matatizo
yanayowakabili katika huduma mbalimbali.
Wananchi wakichanganya Zege kwenye
ujenzi huo.
Watumishi mbalimbali katika Halmashauri ya chalinze
wakijipanga mstari kwaajili ya
kubeba zege kwenyeujenzi huo, mwenye fulana ya bluu na kilemba ni
Afisa mtendaji wa kata ya Mbwewe, Elizabeth Msenga, anaefuatia kulia ni
Afisa kilimo kata ya Mbwewe, Prinscus Mrina.
Mwenye fulana ya njano na kilemba ni Afisa tarafa
kwa ruhombo, Renitha Ruzabico akishiriki
katika ubebaji zege kwenye ujenzi
wa madarasa shule ya msingi Kibindu
Diwani wa
kata ya Kibindu,Mkufya Ramadhani Mawazo
mwenye fulana nyeusi na mistari meupeakiwa katika umwagaji wa zege kwenye
ujenzi huo.
Mkuu wa
wilaya ya Bagamoyo, Alhaji, Majid
Mwanga akiwa juu ya jengo kwaajili ya kumwaga zege.
Baada ya
mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid
Mwanga , kuweka kambi kwa muda
wa siku nne, jengo la vyumba viwili vya
madarasa limefikia hivi.
No comments:
Post a Comment