Wednesday, November 2, 2016

DC. BAGAMOYO ATOA SOMO KWA MADEREVA WA BODABODA MAPINGA, AWACHANGIA LAKI MOJA KWENYE KIKUNDI.



Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Mh. Majid  Mwanga, akikabidhi  shilingi  laki  moja kwa kikundi cha Bodaboda Mapinga, mara baada ya kuzungumza nao.
 ......................................

Mkuu wa wilayaya Bagamoyo ametoa elimu kwa waendesha Bodaboda wa kata ya Mapinga na kuwataka waache kufanya urafiki wa kimapenzi na wanafunzi ili kuwapa nafasi ya kuendelea kimasomo.

Mkuu huyo wa wilaya amesema wanafunziwengi wasichana hutumia usafiri wa bodaboda kufika shuleni ambapo madereva wa bodaboda hutumia nafasi hiyo kuwalaghai kimapenzi hali inayopelekea wanafunzi kukatisha  masomo kwa kupata mimba na vishawishi vingine.

Alisema jamii inahitaji kina mama walioenda shule ili kusimamia vyema  majukumu yao  na kwamba kina mama wanaotarajiwa  ni hawawasichana wa sasa ambao wanakumbana na changamoto za waendesha bodaboda.
Aidha, aliwataka kutoa ushirikiano kuwafichua wale wote wenye tabia hiyo ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Mkuu huyo  wa wilaya aliwachangia shilingi laki moja waendesha boda boda hao katika kikundi  chao ikiwa ni ishara ya kutambua  mchango  wao katika jamii katika kazi wanazofanya huku  akiwasihi  kutovunja sheria  za nchi.




Waendesha bodabodaMapinga wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo mara alipowatembelea na  kuzungumza nao.


No comments:

Post a Comment