Wednesday, November 9, 2016

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA

lic1
Katibu Msaidizi  toka Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma Bw. Peleleja  Masesa akiwaeleza waandishi wa Habari(hawapo pichani) leo Jijini Dar es salaam kuhusu mikakati ya Serikali kuhakikisha kuwa watumishi wa Umma wanazingatia maadili ya Utumishi wa Umma ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.
........................................


Serikali imewataka watumishi wa umma kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma ili kuleta ustawi kwa wananchi kwa kutekeleza mipango  inayolenga kukuza uchumi na kutoa huduma bora.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es salaam na Katibu Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma Bw. Peleleja Masesa wakati wa mkutano na vyombo vya Habari.

Bw. Masesa amesema kuwa Matokeo ya Makosa ya watumishi wa Umma waliokata rufaa Tume ya Utumishi wa Umma mwaka 2014/2015 yanaonyesha kuwa kati ya watumishi 135 walikata rufaa walipatikana na makosambalimbali ambapo 54 walipatikana na kosa la utoro kazini.

Bw. Masesa aliongeza kuwa watumishi wengine 16 walishindwa kutekeleza majukumu yao,10 kumdharau mwajiri,8 kughushi nyaraka mbalimbali,8 kufanya malipo kinyume na taratibu,aidha makosa mengine yalikuwa chini ya watumishi 7.

Aidha Masesa aliwataka watumishi wa Umma kujiepusha na vitendo vya rushwa,ulevi,utoro makazini na matendo yote yanayokwenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

“ Utendaji kazi katika utumishi wa Umma huongozwa na sheria,kanuni,taratibu na Miongozo mbalimbali ambayo ipo”Alisisitiza Masesa.

Pia  Masesa amesema kuwa watumishi watakaoshindwa kuzingatia taratibu zilizowekwa watachukuliwa hatua kali za kisheria na mamlaka za nidhamu katika taasisi husika.

Tume ya Utumishi wa Umma,inawataka waajiri,Mamlaka za ajira na nidhamu na Watumishi wote kuzingatia kanuni za maadili wakati wote wanapotekeleza majukumu yao ili kukuza uchumi,kutoa huduma bora kwa jamii na kulinda amani na utulivu wan chi.lic2

Katibu Msaidizi  toka Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma Bi. Celina Maongezi akisisistiza jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na vyombo vya habari. Kulia ni Katibu msaidizi wa Tume hiyo Bw. Peleleja Masele,kushoto ni Afisa Habari na Mawasiliano wa Tume hiyo Bi Jorlin Kagaruki.
 lic3

Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma uliofanyika leo Jijini Dar es salaam.



No comments:

Post a Comment