Tuesday, November 29, 2016

ASKARI POLISI AFARIKI DUNIA KIBAHA KWA KUJIPIGA RISASI BILA YA KUKUSUDIA.

Askari  Polisi  mwenye namba H.3348 PC  Armand  Evarist  Furaha mwenye umri wa miaka 33 amefariki dunia baada ya kujipiga risasi kwa bahati mbaya.

Taarifa iliyotolewa na  Kaimu kamanda wa  Polisi  Mkoa wa  Pwani, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Blasius Chatanda imesema tukio hilo  limetokea Tarehe 22 Novemba 2016 majira ya saa moja usiku katika eneo  la maili moja sokoni, kata ya maili moja Tarafa ya Kibaha Wilaya ya Kibaha  mkoani  Pwani.

Kaimu Kamanda Chatanda alisema Marehemu alikuwa amepangiwa lindo kwa mkuu wa wilaya ya Kibaha ambapo baada ya kushuka  kwenye Gari  Bunduki ilfyatuka  na  kumjeruhi na  kwamba alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya rufaa ya Tumbi.

SSP Chatanda alisema marehemu alikuwa mbele katika Gari namba PT 1732  lililokuwa likiendeshwa na Askari mwenye namba F. 3064 CPL Grayson na kutaja Bunduki aliyokuwa nayo marehemu aina ya SMG ambayo ilimpiga kifuani upande wa kushoto.  

No comments:

Post a Comment