Posts

DC MTANDA ASITISHA ZABUNIMPYA YA WAKANDARASI WANAOZOA TAKA HADI KUFANYIKA KWA TATHIMINI .

Image
    Mkuu wa wilaya ya Arusha,Said Mtanda akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na sakata hilo jijini Arusha . ************************** Julieth  Laizer ,Arusha Arusha.Mkuu wa wilaya ya Arusha ,Said Mtanda amesitisha  zabuni mpya ya wakandarasi wa kuzoa taka ngumu iliyokuwa ianze agosti mosi  mwaka huu  hadi kufanyika kwa tathimini baada ya kuwepo tuhuma kuna waliopewa zabuni hawana sifa.   Mtanda ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha na ambapo alisema kuwa, amekuwa akipokea malalamiko mbalimbali juu ya wakandarasi hao kusitisha zoezi la ukusanyaji taka kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kushindwa kujua hatma yao kutokana na kuambiwa mikataba yao imeisha.    “Mimi malalamiko hayo niliyapata na ninachotaka kusema hapa ni kuwa nawaomba wakandarasi wote waliokuwa wanazoa taka waendelee na shughuli zao za uzoaji taka kama kawaida hadi pale watakapofanyiwa tathmini  kila mmoja na kuweza kupewa ...

TAASISI YA JAI YAWAFARIJI WAGONJWA KWA MISAADA, SHEIKH MKOA SINGIDA ANENA MAZITO.

Image
  Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro akimuombea dua mmoja wa wagonjwa aliyelazwa kwenye hospitali hiyo. ............................................... Na Dotto Mwaibale, Singida SHEIKH wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro amewaongoza wanajumuiya wa Taasisi Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) kwa kuwapatia msaada wa chakula na vinywaji wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Mandewa. Taasisi hiyo ambayo inajihusisha  kutoa huduma kwa wagonjwa na yatima imetoa misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Sikukuu ya Eid Al-Adha ilyofanyika leo. Akizungumza kabla ya kutoa msaada huo, Sheikh Nassoro alisema jambo linalofanywa na taasisi hiyo ni jambo jema kwani limejaa ucha Mungu na kila mwanajumuiya hiya malipo yake yapo kwa Mwenyezi Mungu. “Hiki mnacho kifanya ni chema mmeacha shughuli zenu, waume zenu, watoto na marafiki badala ya kusherehekea nao sikukuu hii mmeona mje kutoa faraja kwa kuwatembelea hawa wagonjwa kwa kuw...