Wednesday, March 21, 2018

AJALI YA GARI YA MKURUGENZI WA TBC, WAWILI WAFARIKI.


Watu wawili wamekufa wilayani Kasulu mkoani Kigoma katika ajali ya gari la Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Dkt. Ayub Rioba lililokuwa likitokea wilayani Kibondo kwenda Kigoma Mjini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma, Kamishna Msaidizi Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema chanzo cha ajali hiyo ni utelezi uliosababisha gari kuacha njia na kuwagonga waenda kwa miguu watatu.

Gari la Mkurugenzi Mkuu wa TBC lililopata ajali lenye namba za usajili  STK 8769 lilikuwa na abiria wawili akiwemo mkurugenzi mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba na Mkuu wa kanda ya magharibi TBC Mhandisi Zebron Mafuru ambao  wote wametoka salama na hali zao ni nzuri.

Dkt. Rioba yuko katika ziara ya kukagua vituo vipya vya matangazo vilivyojengwa katika maeneo ya mipakani.

No comments:

Post a Comment