Sunday, September 24, 2017

JESHI LA POLISI LAFUNGA MAFUNZO YA UTAYARI CHUO CHA POLISI KIDATU

2
Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto), akizungumza jambo na Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Leonard Paulo (kulia),  muda mfupi kabla ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi.
 1
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Leonard Paulo (katikati),  akiwa ameongozana na Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto) na Mkuu wa chuo cha Polisi Kidatu kilichopo mkoani Morogoro, kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zarau Mpangule, wakati alipowasili katika chuo hicho kwa ajili ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati wanapotekeleza majukumu yao.
 3
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Leonard Paulo, akifanya mazoezi ya viungo na baadhi ya askari wanaoshiriki Mafunzo ya Utayari na kujengewa uwezo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi, mafunzo yanayofanyika katika Chuo cha Polisi Kidatu Kilichopo mkoani Morogoro. 

Picha na Jeshi la Polisi

No comments:

Post a Comment