Tuesday, September 26, 2017

WAZIRI WA AFYA ATOA MIEZI 8 KILA HOSPITALI YA MKOA NA WILAYA KUJENGA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA.



Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto Umy Mwalimu ametoa miezi nane  kwa hospitali za mikoa na wilaya nchi nzima kuhakikisha wananjenga majengo ya kulea huduma za dharula katika hospitali hizo.

Waziri ummy Mwalimu ametoa agizo hilo mjini Bagamoyo, tarehe 25 Septemba 2017, alipokuwa akiweka jiwe la msingi jengo la huduma za dharula na jengo la wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo.

Alisema wananchi wengi wanafariki kabla ya kufika kwa Daktari kutokana na kutokuwepo kwa majengo yanayotoa huduma za dharula katika Hospitali hizo.
alisema anatoa agizo hilo kuhakikisha kila Hospitali ya mkoa na Wilaya inaanza ujenzi wa majengo hayo na mwisho ni tarehe 30 juni 2018 kila Hospitali iwe imekamilisha ujenzi huo.

Ujenzi wa majengo ya huduma za dharula na wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ya Bagamoyo umefadhiliwa na Taasisi ya Dhi nureyn na kwa kushirikiana na wahisani kutoka saudi Arabia 

Aidha, ujenzi huo ambao utagharimu shilingi milioni mia tani unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu.

Wakati huohuo Waziri Ummy Mwalimu alisema amekipandish hadhi kituo cha Afya cha msoga na kuwa Hospitali na kwamba kilichobaki ni kukabidhi rasmi Barua ya kupandisha hadhi kituo cha Msoga.

Awali Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj, majid Mwanga alimuomba Waziri wa Afya, kukipandisha hadhi kituo cha afya ili iwe Hospitali kutokana na kukuwa kwa mji wa Chalinze.

Mkuu wa wilaya pia alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungno wa Tanzania Dkt. john Magufuli kwa kukabidhi majengo yaliyokuwa yanatumika na Tan Roads huko msata ili yatumike kwa Halmashauri ya Chalinze.
Alisema kutokana na kufunguliwa kwa Barabara ya Msata Bagamoyo majengo ayo wanakusudia kufanya kituo cha Afya ambacho kitawahudumia wananchi wa Msata na wapita njia.

Waziri Ummy Mwalimu pia amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo kwa kutafuta wafadhili waliofanikisha ujenzi wa majengo ya huduma za dharula na wodi ya wazazi.
Watendaji kutoka Dhi nureyn, Kamati ya ulinzi na Usalama wilaya ya Bagamoyo pamoja na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Bagamoyo wakifuatilia shughuli ya uwekaji jiwe la msingi katika majengo ya wodi ya wazazi na jengo la huduma za dharula katika Hospitali ya Wilaya bagamoyo.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj, majid Mwanga akizungumza katika shughuli hiyo iliyofanyika viwanja vya Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo.

No comments:

Post a Comment