Wednesday, September 20, 2017

WENYE VYETI FEKI WAJISALIMISHE- KAIRUKI.

SAM_5645

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ,Angella Kairuki ,akizungumza wakati wa mkutano na watumishi wa halmashauri ya Kibaha Mjini na Vijijini pamoja na watumishi wa mkoa wa Pwani kufuatilia zoezi la uhakiki wa vyeti namna lilivyofanyika kwenye mkoa huo,wa kwanza kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo .
...................

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ,Angella Kairuki ametaka ,mshahara wa katibu tawala msaidizi uratibu wa serikali za mitaa sekretarieti ya mkoa wa Pwani ,Martha Nzungu,uondolewe kwenye mfumo wa malipo baada ya kuhakikiwa cheti chake kidato cha nne chenye majina tofauti.

Aidha ametoa rai,watumishi wa umma nchini wanaotumia vyeti vya kughushi ama visivyo vyao wajiondoe wenyewe mara moja katika utumishi wa umma kwani wakiendelea kukaa itawagharimu .

Kairuki ameeleza ,endapo atabainika mtumishi cheti cha magumashi atatakiwa kurejesha mishahara ya miezi yote aliyoiibia serikali.

Aliyasema hayo mjini Kibaha wakati wa mkutano na watumishi wa halmashauri za Kibaha Mjini na Vijijini pamoja na watumishi wa mkoa wa Pwani kufuatilia zoezi la uhakiki wa vyeti lilivyofanyika kwenye mkoa huo.

Alieleza mtumishi huyo anapaswa kuondolewa kwenye orodha ya malipo ya mshahara ili kupisha uchunguzi.

Kairuki alieleza,kuna kila sababu ya kufanya uchunguzi juu ya suala lake la kutumia majina tofauti ya kwenye malipo ya mshahara na jina la kwenye cheti chake.

Alisema cheti chake cha kidato cha nne kipelekwe baraza la mitihani NECTA kwa ajili ya kuhakikiwa .

Hata hivyo Kairuki alipongeza, hatua ya kusimamishwa kwa  Martha Nzungu kutokana na kushindwa kuwasilisha vyeti vya kitaaluma tangu Julai mwaka huu.
 
“jitihada zinazoendelea za uhakiki wa watumishi wa umma bado zoezi hilo limekuwa na dosari kwani kuna baadhi bado wanaendelea kutumia vyeti visivyo vyao,” alisema Kairuki.

“Makatibu tawala wa mikoa wanapaswa kuangalia na kujiridhisha na majina ya watumishi kwenye orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi wa umma na ya kwenye zoezi la uhakiki kama yanafanana”

“Majina yalioonekana kwenye zoezi la uhakiki ndiyo yanayopaswa kuonekana kwenye orodha ya malipo ya mishahara na kama kuna mtumishi hajahakikiwa anatakiwa aondolewe kwenye malipo ya mshahara,” alifafanua Kairuki.

Nae mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo alisema mkoa ulifanya zoezi hilo kama serikali ilivyoelekeza ili kubaki na watumishi wenye sifa na kuwaondoa wale wasio na sifa.

Mhandisi Ndikilo alieleza ,watumishi waliopewa dhamana ya kusimamia mfumo huo wa kuhakiki watumishi wasifanye kazi hiyo kwa kulindana ili kuepuka kuendelea kuwa na watumishi wasio na sifa.

Hivi karibuni ,Martha Nzungu ambae pia ni mke wa katibu tawala (RAS)mstaafu mkoa wa Pwani ,Bernard Nzungu alitakiwa kuwasilisha vyeti vya kitaaluma kwani jina analotambulika kwenye malipo ni tofauti na lililopo kwenye vyeti

No comments:

Post a Comment