Tuesday, August 15, 2017

RAIS WA ZANZIBAR AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA CCM UNGUJA

DSC_0751
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kuashiria Uwekaji wa Jiwe la msingi Jengo la CCM  Tawi Unguja Ukuu Kaebona Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo akiwa katika mwendelezo wa ziara zake katika Mkoa huo
 DSC_0757
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Tawi Jipya la CCM Unguja Ukuu Kaebona Bw.Khatib Ramadhan (wa pili kulia) mara baada ya kuweka Jiwe la msingi Jengo la   Tawi hilo leo  akiwa katika mwendelezo wa ziara zake katika Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja,(kushoto) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Juma Abdalla Juma
 DSC_0898
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akipata maelezo kutoka kwa Nd,Suleiman Haji Suleiman (Mkongo (kushoto) Mkulima wa Ndimu wakati alipofika katika Kijiji cha Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo kutembelea na kukagua Shamba la mkulima huyo akiwa  akiwa katika mwendelezo wa ziara zake katika Mkoa huo
 DSC_0926
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipofuatana na Mkulima wa Ndimu Nd,Suleiman Haji Suleiman Mkongo (wa pili kulia) pamoja na Viongozi wengine walipotembelea Shamba la Mkulima huyo katika Kijiji cha Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo,Rais akiwa katika mwendelezo wa ziara zake katika Mkoa huo.
 DSC_0965
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein   alipokuwa akichuma Ndimu katika Shamba la Nd,Suleiman Haji Suleiman Mkongo (kulia)  wakati alipotembelea Shamba la Mkulima huyo katika Kijiji cha Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo,alipokuwa   katika mwendelezo wa ziara zake katika Mkoa huo,[Picha na Ikulu.] 15/08/2017.

No comments:

Post a Comment