Tuesday, August 22, 2017

CHALINZE YAGAWA PIKIPIKI 14 KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI.

Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani kikwete katikati na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze, Edes Lukoa kulia wakikabidhi Pikipiki kwa watumishi 10 wa Halmashauri hiyo na hivyo kufanya jumla ya watumishi waliopewa pikipiki kufikia 14.

Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete alisema kuwa Halmashauri ya Chalinze imejipanga kuwaondolea adha ya usafiri watumishi wake kwa kuwapatia pikipiki.

Alisema awali walianza kuwapa pikipiki maafisa Mifugo wanne na baada ya kukusanya nguvu ya kutosha wamewapatia pikipiki watendaji hawa 10 ili kukamilisha idadi ya watumishi 14 katika halmashauri. 

Aliongeza kwa kusema kuwa, awamu inayokuja ni kuwaangalia Watendaji Kata zote ili kuweza kuwafikia wananchi waliowachagua na kusikiliza shida zao na kuzitatua.

No comments:

Post a Comment