Tuesday, August 29, 2017

UZINDUZI WA MPANGO MKAKATI WA MAAMBUKIZI YA VVU BAGAMOYO.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mh. Alhajj, Majid Hemed Mwanga,(kushoto), akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Fatuma Omari Latu, (katikati) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally Issah, Wakionesha kitabu kuashiria kuzindua rasmi kwa
Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mh. Alhajj, Majid Hemed Mwanga, akizungumza wakati wa uzinduzi huo jana Agosti 28, 2017. katika Ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.
 ..............................
Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo, umezinduliwa Rasmi hapo jana Tarehe 28 Agost 2017. huku wadau wa mpango huo wakitoka na azimio la utekelezaji ili kufikia malengo yake.

Mgeni Rasmi katika Uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mh. Alhajj, Majid Hemed Mwanga, amesema vita dhidi ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI sio ya mtu maalum, na kwamba kila mtu kwa nafasi yake anapaswa kupambana kwa namna itayosaidia kupunguza maambukizi mapya katika wilaya ya Bagamoyo na hatimae kufikia lengo la kitaifa la asilimia 5.1 

Aliongeza kwa kusema kuwa Serikali inaongeza juhudi ya kupambana na maambukizi mapya kwa kuwashirikisha watu mbalimbali na makundi maalum lengo likiwa ni kufikisha ujumbe utakaosaidia kupunguza maambukizi ya VVU na UKIMWI katika Wilaya ya Bagamoyo.

Aidha, alitumia nafasi hiyo kumuomba Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, kutenga kiasi cha fedha kutoka katika Asilimia 5 za vijana na asilimia 5 za kinamama kuangalia namna ya kuwawezesha watu wanaoishi na VVU ili waweze kuto Elimu kwa makundi mbalimbali kuhusiana na madhara yatokanayo na VVU na UKIMWI lakini pia namna ya kuhamasisha jamii isiweze kuingia kwenye vishawishi vitakavyopelekea maambukizi ya VVU na UKIMWI.

Awali akiwasilisha mada mbele ya Mgeni Rasmi, Mratibu wa Huduma za Ushauri na Upimaji wa VVU Wilaya ya Bagamoyo, Mmanyi Philipo, alisema Tanzania katika kupunguza maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI Kitaifa kutoka asilimia 7% Mwaka 2003-2004 hadi Asilimia 5.1% Mwaka 2011 – 2012:

Aidha, Wilaya  ya Bagamoyo, Kiwango cha Maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI ni Asilimia 5.9% ambacho ni kikubwa zaidi kuliko kiwango cha Maambukizi ya VVU Kitaifa ambacho ni Asilimia (5.1%).
 
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mh. Alhajj, Majid Hemed Mwanga,(kushoto) akipokea kitabu kutoka kwa Afisa Vijana wilaya ya Bagamoyo, Hellen E. Kisanji, kwaajili ya uzinduzi wa Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo, wanaoshuhudia wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally Isaha, na wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Fatuma Omari Latu.
   Mratibu wa Huduma za Ushauri na Upimaji wa VVU Wilaya ya Bagamoyo, Mmanyi Philipo, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo.
 Afisa Mwitikio wa Taasisi za Umma Dr. Hafidh Ameir, kutoka Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania,(TACAIDS) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo.
 Meza kuu, wa pili kushoto ni mgeni Rasmi (katika) uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mh. Alhajj, Majid Hemed Mwanga, wa kwanza kushoto ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Fatuma Omari Latu wa tatu kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo Ally Ally, wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo.
Wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo, Erica Yegela, wa pili ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP. Adam Amani Maro, wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo.
 Makamo Menyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Saidi Ngatipula.
Washiriki kutoka asasi mbalimbali za kiraia.
Watumishi wa Halmashauri ya Bagamoyo.


Picha ya pamoja Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Mh. Alhajj, Majid Hemed Mwanga,(mwenye tai katikati) na washiriki wa mkutano huo wa kuzindua Mpango Mkakati juu ya Maambukizi ya VVU na UKIMWI wa Wiayani Bagamoyo.

No comments:

Post a Comment