Tuesday, August 15, 2017

SKAUTI 200 KUTOKA UINGEREZA WATEMBELEA TANZANIA.

 Jumla ya skauti wapatao 200 kutoka jimbo la Hamshire Uingereza wapo nchini Tanzania kwa ziara ya kazi za jamii pamoja na skauti wenzao wa Tanzania.

Skauti hao wamekuja nchini kwa ajili ya kufanya kazi za jamii ambapo wamejitolea kukarabati Kambi kuu ya Mafunzo ya Skauti iitwayo Bahati ambayo ipo mkoani Morogoro nje kidogo ya mji huo.

Ziara hiyo ambayo  itachukua zaidi ya mwezi mmoja kukarabati eneo hilo la kambi, na baada ya hapo watatembelea maeneo mengine ya Kilosa, Ifakara, na Mikumi kabla ya kurejea nchini kwao Uingereza.

Kazi za kujitolea kwa vijana Skauti ni mojawapo ya shughuli zao za kila siku kusaidia watu siku zote kama Kanuni za Skauti zinavyosema.

Hii ni mara ya kwanza kwa kundi kubwa la Skauti kutoka Uingereza kutembelea Tanzania.

Wakiwa nchini Tanzania skauti hao kutoka nje wanashirikiana na wenyeji wao Chama cha Skauti Tanzania, kutoka Makao Makuu D’salaam na wengine wa mkoani Morogoro.

HIDAN .O. RICCO.
KAMISHNA MKUU MSAIDIZI
MAWASILIANO NA HABARI
(0673 019112)
MHESHIMIWA JAKAYA AKIWA NA SKAUTI KTK MKUTANO MKUU WA DUNIA 2017

No comments:

Post a Comment