Saturday, August 12, 2017

BANDARI BUBU BAGAMOYO KUDHIBITIWA.

IMG_20170727_130233
Jeshi la Polisi mkoani Pwani limesema limejipanga kudhibiti Bandari bubu zilizopo Bagamoyo ili kukomesha Biashara ya kusafirisha kutoka nje ya nchi kinyume na utaratibu,

Akizungumza na waandishi wa Habari Ofisini kwake Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Jonathan Shanna, alisema Bagamoyo pekee ina Bandari bubu 18 na kwamba miongoni mwa njia zinazotumika kupitisha wahamiaji wa kigeni bila ya kufuata utaratibu ni pamoja hizo.
 
Aidha, Kamanda Shanna alisema Jeshi la polisi mkoani Pwani limejipanga kudhibiti njia zote za panya zinazotumika kupitisha magendo ya aina mbalimbali. 
 
Kamanda Shanna alitoa kauli hiyo wakati akitoa Taarifa kuhusu wahamiaji 72 walioingia nchini kinyume cha sheria ambao walikamatwa hivi karibuni katika shamba la Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO)huko Vigwaza wilaya ya kipolisi Chalinze.
 
Kamanda Shanna ,amesema kuanzia sasa.watataifisha mali zote za watu wanaojihusisha na biashara ya usafirishaji wa wahamiaji haramu.

Aidha amewatahadhalisha wale wanaotoa vyombo vyao vya majini na nchi kavu kusafirisha wahamiaji hao  kwani navyo vitataifishwa .

Alisema wanaojihusisha kusaidia na kuwawezesha kufika wahamiaji haramu watawachunguza mali mbalimbali walionazo kama imetokana na utakatishaji fedha na endapo itabainika imetokana na biashara hiyo zitafilisiwa.

Kamanda Shanna alibainisha,wataiomba mahakama kutaifisha mali zote za wale watakaobainika kuhusika kupata mali hizo na fedha na biashara haramu.

Alisema sheria ipo wazi inasema watu hao wapewe kifungo ama kupigwa faini hivyo itapendeza na itafurahisha jeshi la polisi kama watakuwa wanapewa adhabu zote na kufungwa .

Kamanda Shanna ,alisema taarifa ikifika kwao kuwa wanafungwa na kupewa adhabu kali ndipo wataacha kuingia nchini kwani watajua Tanzania sio mahala pa mchezo wala kukimbilia.

“Hii kuwakamata kuwapiga faini na kuwarudisha kwao ndio maana wanafanya mchezo mchezo kukimbilia huku,ukiwapiga faini wanakwenda wanarudi ni mchezo wa kuigiza”alisema .

Kamanda Shanna alielezea kwamba,Tanzania ina sheria zake endapo sheria zitawabana wahamiaji hao na kukoma kugeuza nchi kuwa lango lao la kupita kwenda nchi jirani ikiwemo Afrika ya kusini.
 
Hata hivyo ,kamanda huyo alisema wahamiaji waliokamatwa wameshawafikisha ofisi ya uhamiaji mkoani Pwani na watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Pamoja na hilo,Kamanda Shanna alisema wanafanya oparesheni kusaka wahalifu mbalimbali ,zoezi ambalo ni endelevu.

No comments:

Post a Comment