Tuesday, August 15, 2017

SHULE YA MWASAMA YAPEWA TUZO NA UMOJA GROUP YA UJERUMANI.

Mkurugenzi wa shule ya msingi MWASAMA, Mwajuma Saidi Masaigana, kushoto akipokea tuzo maalum kutoka kwa Umoja Group ya nchini Ujerumani, mara baada ya kutembelea shuleni hapo na kufurahishwa na namna shule hiyo inavyowaandaa watoto katika kupata Elimu bora huku wakiwa katika mazingira mazuri ya kujifunzia, anaemkabidhi zawadi hiyo kulia ni Mwenyekiti wa umoja Group, Veronika Tereh.
 Baadhi ya wanakikundi cha umoja Group kutoka nchini Ujerumani, wakiwa kwenye jukwaa ambapo waliimba wimbo unaohimiza umoja kwa lugha kiswahili, wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika shule ya msingi MWASAMA, mara walipotembelea shuleni hapo, Mwenye shati ya njano katikati ni
Mwenyekiti wa umoja Group, Veronika Tereh.
    
Mkurugenzi wa shule ya msingi MWASAMA, Mwajuma Saidi Masaigana, akiwa na wageni waalikwa meza kuu wakati wa kuwakarisha wageni wa Umoja Group kutoka nchini Ujerumani walipotembelea shuleni hapo.
   
Sehemu ya wgeni kutoka nchini Ujerumani wakiangalia burudani iliyokuwa ikitolewa na wanafunzi wa shule ya MWASAMA.
 wageni wa Umoja Group kutoka nchini Ujerumani wakipata vinywaji mara kumaliza kufanya mazungumzo na wenyeji wao walipotembelea shule ya msingiMWASAMA iliyopo mjini Bagamoyo.
 Afisa Utamaduni wilaya ya Bagamoyo, Hamisi kim, (kushoto) alipowasili katika shule ya msingi MWASAMA ili kushiriki hafla fupi ya kuzungumza na wageni wa kikundi cha Umoja Group kuoka nchini Ujerumani walipotembelea katika shule ya MWASAMA, kulia ni Mratibu wa shughuli hiyo, ambae pia ni mjumbe wa bodi ya shule, Hamza Mfaume.
 Mkurugenzi wa KAYA FM. RADIO ya mjini bagamoyo, Marie Shaba, akizungumza na wageni kutoka nchini ujerumani katika hfla fupi ya kuwapokea iliyofanyika shule ya Msingi MWASAMA mjini Bagamoyo.
 Mjumbe wa kamati ya CCM wilaya ya Bagamoyo, Mwinyi Hashim Akida, akizungumza na wageni hao, kushoto ni Mwalimu John Mponda kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)
 
Wageni hao walipata fursa ya kutembelea eneo la shule ambapo ndani yake walijionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na shule hiyo ikiwemo ufugaji wa Samaki kama hapa wanavyoangalia Samaki waliofugwa kwenye Bwawa.

No comments:

Post a Comment