Friday, January 27, 2017

MADIWANI BAGAMOYO WAPITISHA BAJETI YA BILIONI 41 KWA MWAKA WA FEDHA 2017/18.



Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aliy Aliy.
......................................
Baraza la Madiwani la Halmashauri  ya Bagamoyo imepitisha Bajeti ya bilioni 41 kwa mwaka wa fedha 2017/18 ikiwa na  ongezeko la aslilimia 14 ukilinganisha na bajeti  ya mwaka 2016/17.

Awali  akiwasilisha Bajeti hiyo Afisa Mipango wa Halmashauri ya Bagamoy, Malboard Kapinga amesema malengo ya bajeti hiyo ni mapato  kutoka makusanyo ya ndani, Ruzuku kutoka Serikali  kuu pamoja na wahisani mbalimbali.

Baada ya  kuwasilishwa kwa Bajeti hiyo  wajumbe wa kikao hicho wamepitia bajeti hiyo ukurasa kwa ukurasa na hatimae kujiridhisha na kuipitisha Bajeti hiyo ambapo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aliy Aliy, amesema Baraza hilo limeridhia Bajeti hiyo.

Mwenyekiti huyo  wa Halmashauri ya Bagamoyo, amesema Bajeti hiyo ya Bilioni 41 inawalenga wananchi wa Bagamoyo na kwamba kazi  kubwa  ya madiwani  ni  kusimamia ukusanyaji  wa  mapato na kuhakikisha zinakwenda kwenye utekelezaji  wa miradi ya maendeleo


No comments:

Post a Comment