Monday, January 23, 2017

RAIS DK. MAGUFULI AMPOKEA RAIS ERDOGAN WA UTURUKI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

13
Msafara wa Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan akiwa na 
 mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Magufuli wakielekea kwenye ukumbi wa mkutano leo mara baada ya kuwasili Ikulu.
 021

Msafara wa Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan ukiwasili katika viwanja vya Ikulu leo wakati alipopokelewa na mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Magufuli leo katika Ikulu ya Magogoni  jijini Dar es salaam , Rais huyo yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
 2

Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan akisalimiana na Mkuu wa Majeshi Jenerari Davis Mwamunyange  katika viwanja vya Ikulu leo wakati alipopokelewa na mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Magufuli leo.
 3

Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan aki mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Magufuli leo wakati alipopokelewa kwenye viwanja vya ikulu jijini Dar es salaam.
 4

Msafara wa Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan  na mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Magufuli leo wakipokea heshima kwa kupigiwa nyimbo za mataifa haya mawili na mizinga.
 512

Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan akikagua gwaride  katika viwanja vya Ikulu leo wakati alipopokelewa na mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Magufuli leo.


Serikali ya Tanzania na Serikali ya Uturuki zimesaini mikataba tisa ya makubaliano ya kiuchumi inayolenga katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa maendeleo baina ya nchi hizo.

Mikataba hiyo inahusisha sekta za uchukuzi, mawasiliano, habari, elimu, utalii, utafiti, viwanda, afya na ulinzi.

Akizungumza mara baada ya kusaini kwa mikataba hiyo  leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli alisema ujio wa Rais wa Uturuki na ujumbe wake ni kielelezo cha ukuaji wa mahusiano baina ya Tanzania na Uturuki katika nyanja ya biashara na kimaendeleo baina nchini hizo.

Rais Magufuli alisema katika mazungumzo yake aliyofanya na Rais Recep Erdogan kuhusu ujenzi wa Reli ya Standard Gauge nchini, alimjulisha kiongozi huyo kuwa miongoni mwa wakandarasi walioomba zabuni ya ujenzi wa reli hiyo kuwa ni kampuni kutoka Uturuki, hivyo endapo itashinda zabuni hiyo itasaidia kukuza uhusiano uliopo baina ya nchi hizi mbili.

Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa, Serikali ya Tanzania inatarajia kuomba  mkopo kupitia Benki ya Exim ya Uturuki katika kujenga sehemu ya kipande cha ujenzi wa reli hiyo.

Rais magufuli alisema Tanzania inaendelea kunufaika na uwepo wa Shirika la Ndege la Uturuki kwa kufanya safari zake za moja wka moja kutoka nchini Uturuki, kwa kuwa utasaidia kuongezeka kwa idadi ya watalii nchini na hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo.

Kwa upande wake Rais wa Uturuki, Recep Erdogan alisema kuwa uwepo wa mikataba hiyo baina ya Tanzania na Uturuki itasaidia kupata matokeo mazuri ya uhusiano pamoja na fursa mbalimbali za ushirikiano katika nyanja ya Kilimo, Utalii, Ulinzi, Reli ambazo zitawezesha kukuza uchumi wa mataifa hayo.

Rais Erdogan alisema kuwa Uturuki imelenga kukuza ushirikiano uliopo baina yake na  Tanzania kupitia makongamano ya wafanyabiashara yenye malengo ya kukuza uchumi, kuongeza ajira pamoja na kukuza ujasiriamali baina ya Tanzania na Uturuki.

“Kiwango cha Biashara ya uwekezaji katika nchi ya Uturuki ni Dola za kimarekani 150 ambapo lengo letu ni kufika Dola za kimarekani 500” alisema Rais huyo.

Aidha Rais Erdogan alisisitiza kuwa kufanya kazi kwa pamoja kutasaidia nchi hizi kusonga mbele na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali.

Nae Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe alisema kuwa makubaliano ya mkataba baina ya Tanzania na Uturuki katika Sekta ya Utalii yatasaidia katika kutangaza vivutio vilivyopo nchini, kubadilishana wataalamu, kubadilishana taarifa na kuongeza idadi ya watalii nchini.

Prof. Magembe aliongeza kuwa makubaliano hayo yatakuza sekta ya utalii katika kuvutia uwekezaji wa katika maeneo ya hoteli, fukwe na mbuga za wanyama zilizopo nchini. 
 7

Wakuu wa vikosi vya iulinzi na usalama wakisubiri kupokelewa kwa Rais wa Uturuki Mh. Recept Tyyip Erdogan.
 9

Makamu wa Rais Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa wakati wa mapokezi hayo.

 10

Baadhi ya mawaziri na watendaji wa serikali ya Uturuki wakiwa wamekaa katika viwanja vya Ikulu.11

Waziri wa Sheria na Katiba Dk. Harrison Mwakyembe kulia akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe wakati wa mapokezi ya Rais wa Uturuki Mh. Recept Tayyip Erdogan.

No comments:

Post a Comment