Friday, January 6, 2017

DC. BAGAMOYO APOKEA MABATI 2,000 KUTOKA SAYONA GROUP.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo amepokea mabati elfu mbili yenye thamani ya shilingi  milioni 40 kutoka  kwa Kampuni ya Sayona  Group ili kusaidia  ujenzi  wa madarasa katika wilaya ya Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya  kupokea msaada huo, Mkuu  wa wilayaya Bagamoyo, Majid  Mwanga, alisema  anaishukuru  Kampuni ya  Sayona Group  kwa kutoa  msaada huo  ambao  utasaidia katika ujenzi wa vyumba vya  madarasa  wilayani humo.

Alisema kwa sasa wilaya ya Bagamoyo imeweka mikakati ya kuongeza vyumba vya madarasa kila kata ili  kuondoa  uhaba wa vyumba vya madarasa  ambapo kwa sasa limekuwa changamoto kubwa.

Aliongeza kuwa mara baada  ya  kukamilisha utengenezaji  wa madawati  nguvu zote zim eelekezwa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Katika  mikakati hiyo  ya ujenzi wa madarasa  wilayani Bagamoyo, Mkuu wa wilaya hiyo, Majid  Mwanga amekuja na  kauli  mbiu  isemayo    "UONGOZI  UNAOACHA  ALAMA"   ambapo kwa kushirikiana na viongo wake  mbalimbali Ngazi  ya Tarafa, Kata, Vijiji na Vitongoji  wananchi  wamekuwa wakishiriki ilikufanikisha ujenzi huo.

Aidha,  alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuchangia ujenzi huo wa madarasa wialyani  humo ili kuleta dhana ya  ushirikishwaji  wa  maendeleo kati ya  wan anchi na serikali.

Kwa upande wake  Mkurugenzi  msaidizi  wa  Kampuni ya  Sayona Group ,Aboubakari  Mlawa alisema  wamefikia uamuzi  wa kutoa  msaada huo lengo  likiwa ni  k ui sai dia  serikali  katika  kuleta  maendeleo ambayo  wan ufaika wakubwa  ni wananchi  wenyewe.

Aliongeza  kwa  kusema  kuwa  Kampuni ya Sayona Group  ambayo  inajenga  kiwanda cha Juisi kataya  Msoga wilayani  Bagamoyo , ina wajibu  wa kusaidia miradi m balimbali ya  maendeleo kwakuwa kamapuni hiyo ni  sehemu ya Bagamoyo. 

 Mkurugenzi msaidizi wa Kampuni ya Sayona Group,  Aboubakari Mlawa, akizungumza mara baada ya  kukabidhi mabati hayo.

No comments:

Post a Comment