Friday, November 3, 2023

ONDOENI WASI, NCHI IMEHIFADHIWA VIZURI-KIKWETE

 

Maneno hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofis ya Rais Utumishi na Utawala Bora baada ya ziara ya Kamati ya kudumu Bunge inayosimamia Utawala , Katiba na Sheria kutembelea idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa , Dodoma.



Akizungumza mbele ya kamati Mhe. Kikwete pamoja na kuishukuru kamati kwa kufanya ziara ameeleza kuwa ofisi yake itasimamia na kutekeleza maelekezo yote kwa kuwa tayari Serikali imeshatoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika Idara hiyo na mrejesho utatolewa kwa mujibu wa utaratibu mapema iwezekanavyo.


“Ujio wenu hapa umeambatana na maelekezo muhimu sana kwetu ili kuimarisha shughuli zinazofanywa na Idara hii kwa ustawi wa Serikali na Taifa kwa jumla, nasi tuko tayari kutekeleza maelekezo hayo kwa haraka na ufanisi” alisema Mhe. Kikwete.


Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Dkt. Mhagama amemsisitiza Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuhakikisha ofisi yake inaisimamia vyema Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa katika zoezi la kuhifadhi nyaraka ambazo zimekusanywa hivi karibuni ili ziwe kwenye utaratibu mzuri kama zilivyo nyingine kwa lengo la kuepuka upotevu wowote wa nyaraka hizo. 


No comments:

Post a Comment