Thursday, November 9, 2023

HALMASHAURI YA BAGAMOYO YAVUKA MALENGO UKUSANYAJI WA MAPATO

 

Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo imevunja rekodi ya kukusanya kiwango katika kipindi cha Robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/24 kuaniza Julai mpaka Septemba 2023


Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya Bagamoyo Mhe. Halima Okashi katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika leo tarehe 09 Novemba 2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya.



Akizungumza katika kikao hicho cha Baraza la Madiwani Mkuu huyo wa Wilaya aliwapongeza Madiwani na Watumishi wa Halmashauri hiyo kwa kazi nzuri ya ukusanyaji wa mapato katika kipindi cha Robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/24 kuanzia Julai mpaka Septemba 2023. 



Katika kipindi hicho Halmashauri imekusanya zaidi ya shiling bilioni 1 sawa na asilimia 27.7 ambapo ni asilimia 2.7 zaidi ya malengo waliyojiwekea ya asilimia 25.



"Niwapongeze Madiwani wa Kata zote pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Bagamoyo kazi nzuri ya ukusanyaji wa mapato kwenye taarifa yenu inaonyesha mapato yaliyopatikana ni asilimia 27.7 ambapo malengo yalikuwa ni asilimia 25 hivyo hongereni sana kwa ongezeko hilo la asilimia 2.7" alisema Bi Halima Okashi


Aidha Mkuu wa Wilaya huyo aliwataka Madiwani na Watumishi wa Halmashauri hiyo kuongeza ubunifu zaidi ili kuweza kupata wigo wa kuongeza mapato utakaopelekea uboreshaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo akipokea pongezi hizo kwa niaba ya Baraza la Madiwani Mhe. Mohamedi Usinga aliahidi kuendelea kuboresha vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuboresha mapato kwenye Halmashauri hiyo.





No comments:

Post a Comment