Wednesday, November 15, 2023

EDU KWANZA WATOA FURSA YA MASOMO KWA VYUO VIKUU VYA CANADA & USA KWA WANAFUNZI WA TANZANIA

 

Na Andrew Chale, Dar es Salaam.


EDUKWANZA Consultants Limited ambao ni Mawakala wa Vyuo vya nje ya Nchi kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya ushauri huduma za Wanafunzi ya ILLUME imeendesha zoezi kwa Wanafunzi wa Tanzania kupata fursa za masomo katika Vyuo vya nchi za Canada na Marekani (USA) tukio lililofanyika Jijini Dar es Salaam mapema leo Novemba 15,2023.


Akizungumza katika tukio hilo lililowakutanisha wanafunzi mbalimbali waliofika kupata muongozo sahihi wa Vyuo vya nje, Mkurugenzi wa Edukwanza, Bw. Sarfraz Kassam amesema taasisi yao hiyo ina ushirikiano na Vyuo zaidi ya 500 Duniani ikiwemo Vyuo hivyo vya Canada na Marekani.


"Edukwanza Consultants Limited leo Novemba 15,2023 tumefanya maonesho ya kuvinadi Vyuo vya Canada na Marekani katika mpango wa ‘Study in Canada & USA Fair 2023 ambao unasaidia kutoa fursa kwa in wanafunzi kusoma nje.


Wanafunzi mbalimbali wa Tanzania wamefika na kupata ushauri kutoka kwa Wawakilishi wa vyuo hivyo vya nje, wakipata ushauri wa kujiunga na vyuo hivyo, namna ya kupata visa za masomo, ama namna ya masomo ya kuchagua na muongozo mwingine kwa ajili ya taaluma yao." Amesema Sarfraz Kassam

 





Aidha, amesema kuwa, Vyuo hivyo vya Canada na Marekani ni miongoni mwa vyuo bora na wanafunzi wamepata namna bora ya kupata ushauri wa jinsi ya kuomba kusoma kwenye vyuo hivyo.


Lakini pia amewataka wanafunzi hao kuweza kupitia mitandao ya kijamii ya Edukwanza kupata muongozo sahihi kwa ajili ya hatma yao ya kuchagua Vyuo bora nje ya Nchi.


Edukwanza ni miongoni mwa Mawakala wa Vyuo vya nje ya Nchi iliyosajiliwa na Tume ya vyuo vikuu nchini (TCU) imekuwa kinara katika kunadi na kuongoza kushauri wanafunzi kwenda kusoma nje.


No comments:

Post a Comment