Wednesday, November 1, 2023

ASKOFU BAGONZA: KUWENI NA TABIA YA KUANDIKA HISTORIA ZENU MKIWA HAI.

 

Na Alodia Babara.


Karagwe. 


Askofu wa kanisa la kiinjili la kirutheri Tanzania Dayosisi ya Karagwe Benson Bagonza ameisihi jamii ya watanzania kuwa na tabia ya kuandika mambo yao wakiwa bado wako hai badala ya kusubili waandikwe na watu wengine baada ya kuwa wameaga duniani.


Askofu Bagonza ameyasema hayo Oktoba 31, 2023 katika hafla ya uzinduzi wa kitabu cha mzee Clement Nsherenguzi (87) mkazi wa kata ya Bugene wilaya ya Karagwe.


Bagonza amesema kuwa, baadhi ya watu wanaogopa kuandika historia zao wakiwa bado wako hai badala yake wanasubili kuandikwa na watu wengine, jambo ambalo siyo jema kwani wanapoandika wenyewe inatoa mwanya mpana kwao kipi waandike na kipi wasiandike.


Anatolea mfano wa aliyekuwa katibu muhtasi wa Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere aliyejulikana kwa jina la Joan Wicken ambaye alisha kufa na kabla ya kifo chake alipanga kuandika historia ya hayati baba wa Taifa kwa kutumia kumbukumbu mbalimbali zilizokuwa zinahifadhiwa (dayaries) lakini akasita na kusema historia hiyo itaandikwa baada ya miaka 30.


"Maisha yetu kama wanadamu ni kitabu, lakini kile kitabu kina mambo yaliyoandikwa na ambayo hayajaandikwa na mengine hayaandikiki, nilipewa mwaliko kwenda mjini London kuzindua kitabu cha hayati baba wa Taifa sikwenda lakini kitabu hicho kilizinduliwa siku ya Nyerere day Oktoba 14, 3023 na kitabu hicho kilipangwa kuandikwa na aliyekuwa katibu muhtasi wake kutokana na kumbukumbu mbalimbali za hayati Julius Kambarage Nyerere lakini alisita na kusema kiandikwe baada ya miaka 30 alisubili watu wengi waliomfahamu baba wa Taifa watoweke" amesema askofu Bagonza 


Bagonza amesisitiza upendo na amani miongoni mwa wanajamii na kuwataka kuacha chuki, kwani kufanya hivyo wataongeza miaka ya kuishi kama mzee Nsherenguzi


Aidha mzee Clement Nsherenguzi (87) ametaja lengo la kuzindua kitabu hicho chenye sura 19 na kurasa 163 kuwa ni kuweka kumbukumbu za maisha yake na vitu alivyofanya kwa faida ya jamii na kizazi chake na kimechapishwa 2023 na Tanzania Educational Publishers Ltd (TEP).


Kwa upande wake rafiki wa mzee Nsherenguzi ambaye pia ni mkurugenI wa kampuni iliyochapisha kitabu hicho Pius Ngeze amesema kuwa, wazo la kuandika kitambu lilitolewa na Hope binti yake mzee Nsherenguzi na kukubaliwa kisha mzee huyo alianza kuandika na hatimaye kitabu hicho kikazinduliwa jana. 





No comments:

Post a Comment