Wednesday, November 8, 2023

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA BAGAMOYO LAFANYA KIKAO CHAKE CHA KWANZA CHA ROBO MWAKA 2023

 

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo leo tarehe 8 Novemba 2023 limekutana na kufanya Kikao chake cha kwanza katika mfululizo wa vikao viwili vya Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo, vikao ambavyo vimepangwa kufanya tarehe 8-9 Novemba 2023.

Katika Kikoa hicho Baraza lilipokea Taarifa za Utendaji kwenye ngazi ya Kata kwa robo ya kwanza ya mwaka 2023.

Akipokea taarifa hizo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Mohemed Usinga aliwapongeza na kuwashukuru Waheshimiwa Madiwani wa Kata zote kwa kazi nzuri walizozifanya katika kipindi hiki cha robo ya kwanza.

Aidha Mwenyekiti huyo aliagiza Madiwani pamoja na watendaji wa kata zote kutoanzisha miradi mipya ya maendeleo mpaka miradi iliyopo ikamilike, "Waheshimiwa Madiwani pamoja na Watendaji wa Kata hakikisheni mnamaliza miradi yote iliyokuwa haijakamilika kabla ya kuanzisha miradi mingine, tuhakikishe kwenye kata zetu tunamaliza viporo vyote vya miradi inayoendelea" alisema Mhe Usinga

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw. Majid Mhina alipokea maelekezo ya Baraza hilo na kwenda kuifanyia kazi. "Tumepokea maelekezo ya Baraza kwa ushirikiano wa Idara zetu na wataalamu tulio nao tunaenda kuyafanyia kazi" amesema Bw. Mhina 






No comments:

Post a Comment