Saturday, October 7, 2023

SERIKALI ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA KANISA KATOLIKI - DKT. MPANGO.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema serikali itaendelea kufanya kazi na kushirikiana vema na Kanisa Katoliki pamoja na madhehebu mengine ya dini hapa nchini.
 
Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa mapokezi ya Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa yaliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam akitokea Vatican alipopewa hadhi ya Ukardinali. Amempongeza Kardinali Rugambwa kwa kuendelea kuhubiri amani na umoja wa Watanzania na kumsihi kuendelea kuwa chachu ya amani, upendo na umoja. Makamu wa Rais amesema ni baraka kwa Taifa la Tanzania kupata Kardinali wa tatu.
 
Kwa upande wake Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa amewaomba watanzania wa kila dini kuendelea kumuombea ili aweze kufanya vema kazi hiyo kwa uaminifu na kuweza kuleta maendeleo ya mwanadamu kwa ujumla kuanzia hapa nchini kimwili na kiroho na baadaye hata nje ya nchi.
 
Kardinali Rugambwa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Kanisa, Serikali na watanzania wote waliomtia moyo na kumtumia jumbe mbalimbali za pongezi zilizompa moyo na kumuimarisha.
 
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
06 Oktoba 2023
Dar es salaam. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimsalimiana na Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa mara baada ya Kardinali Rugambwa kuwasili nchini katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam akitokea Vatican alipopewa hadhi ya Ukardinali. (Tarehe 06 Oktoba 2023)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akifurahia jambo na Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa mara baada ya kumpokea alivyowasili nchini katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam akitokea Vatican. (Tarehe 06 Oktoba 2023).


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa pamoja na viongozi wengine wa Kanisa Katoliki wakati wa Mapokezi ya Kardinali Rugambwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Vatican alipopewa hadhi ya  Ukardinali. (Tarehe 06 Oktoba 2023)


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akizungumza na Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa,Maaskofu pamoja na viongozi wengine wa Kanisa Katoliki wakati wa mapokezi ya Kardinali Rugambwa yaliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. (Tarehe 06 Oktoba 2023).


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na Mwadhama Kardinali Protase Rugambwa, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Askofu Gervas Nyaisonga,Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania Askofu Mkuu Angelo Accattino pamoja na viongozi wengine wa Kanisa Katoliki wakati wa mapokezi ya Kardinali Rugambwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere

No comments:

Post a Comment