Sunday, October 22, 2023

SERIKALI YA DKT SAMIA INAWAJALI NA KUWAPENDA WALIMU-DKT JAFO

 

Kisarawe Pwani


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira (Mb) Mhe Dkt Selemani Saidi Jafo amewataka Walimu wote nchini hasa wanawake kuendelea kulea Watoto katika maadili mema zaidi hasa wanapokua shuleni,


Akizungumza Leo 21.10.2023 Mkoa wa Pwani Wilaya Kisarawe katika mafunzo ya walimu wanawake ambapo alisisitiza walimu hao kuendelea malezi Bora ya kuwalea vijana katika Maadili mema,


*"Ndugu zangu katika Utumishi wa Umma ukitaka kuona utukufu wa mwenyezi Mungu basi kuwa Mwalimu maana katika ualimu unafundisha utukufu na ufalme wa Mwenyezi Mungu kwa vijana*" alisisitiza Mhe Dkt Jafo,


Nae kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Kisarawe Mhe FATMA NYANGASA akizungumza katika mafunzo hayo aliwatoa hofu na mashaka walimu kwa kuwaambia Kuwa serikali ya awamu ya sita ya Rais Dkt Samia ni sikivu,


*"Ndugu Walimu tumeyasikia yote yaliosomwa katika Risala na Katibu wenu mengi serikali inayafanyia kazi na mengine yameshafanyiwa kazi hivyo tumuombe Dua Rais wetu apate afya njema na nguvu katika kutatua Changamoto za Watumishi wakiwemo Walimu alisisitiza Mhe Nyangasa,*"


Mafunzo haya kwa Walimu wanawake wote wa Kisarawe yameratibiwa na Chama Cha Walimu Kisarawe kwa Ufadhili wa taasisi mbalimbali za Kisarawe ambapo wameweza kutoa mafunzo katika afya ya akili,ujasiriamali Nk kwa walimua hao zaidi ya mia Tano. 


No comments:

Post a Comment