Tuesday, October 3, 2023

MNKONDYA AFURAHISHWA NA KASI YA UKUAJI WA VANILLA UNUNIO DAR

 


Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.


MKURUGENZI Mkuu wa Makampuni ya Kimataifa ya kilimo cha Vanilla Duniani, Simon Mnkondya amefurahishwa na kasi ya ukuaji wa Vanilla katika shamba lililopo Ununio beach, Dar Es Salaam ambalo limeanza kutoa maua na ustawi mzuri. 


Mnkondya amefanya ziara katika shamba hilo akiwa ameambatana na Mke wake Mama Simon Mnkondya Bi. Upendo Ayo, imekuwa ziara yenye matumaini makubwa hasa baada ya kuona kasi ya ukuaji huo wa vanilla.


"Kwetu Vanilla ni zao lisilo na pingamizi kwenye ukuaji.

Soko na bila shaka linabakia kuwa zao la kwanza kwa bei Tanzania na kuwa Vanilla ni zao la pili kwa bei duniani" Amesema Mnkondya.


Aidha,ameongeza kuwa hatua hiyo inapelekea kupigia debe kubwa zao hilo la Vanilla ili ikiwezekana kiwe kilimo cha Taifa.


"Hichi kwetu ni kitu kinachotufanya tulipigie debe kubwa zao la vanilla na ikiwezekana kiwe ni kilimo cha Taifa kwa vile zaidi ya asilimia 80 ya nchi yetu Tanzania Vanilla inamea na kufanya vizuri ikiwa njia za kisasa za 'Greenhouses' na umwagiliaji wa matone zitatumika." Amesema Mnkondya.


Aidha, Mnkondya amesema kuwa, Shamba la Ununio ni shamba lililobezwa kwa sababu ya uwepo wa karibu na mchanga wa bahari mahali hapo lakini umakini wa kampuni ya Vanilla International Limited limekuwa shamba darasa kwa Dar Es salaam."Amesema Mnkondya


Hata hivyo, Mkurugenzi amewaasa wana Ununio na Dar Es salaam kuweza kutembelea kurasa za kampuni hiyo kwenye mitandai yao ilikuwezeshwa namna sahihi za ulimaji wa zao hilo.


No comments:

Post a Comment