Sunday, October 1, 2023

WAZIRI MKUU, MAJALIWA AMPA RUNGU RC PWANI KUNYANG'ANYA VIWANJA VILIVYOMILIKIWA NA WAWEKEZAJI KWA MUDA MREFU BILA KUENDELEZWA.

 

Na Scolastica Msewa, Mafia.


Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassimu Majaliwa amempa rungu Mkuu wa mkoa wa Pwani Mheshimiwa Abubakari Kunenge kunyang'anya Visiwa na viwanja uwekezaji wa Utalii Wilayani Mafia vilivyong'ang'aniwa na wawekezaji miaka mingi bila kuendelezwa kwa kutofanya chochote ili vigawiwe kwa wawekezaji wengine.


Amesema hayo wakati akifunga siku tatu za maonyesho ya uwekezaji wa katika uchumi wa buluu na kutangaza Utalii mazao ya bahari katika kisiwa cha Mafia mkoani Pwani Mheshimiwa Majaliwa amesema hatua hizo zifanyike kwa kuzingatia taratibu na Sheria za nchi kwani muda wa mwekezaji kumiliki eneo la uwekezaji bila kuendeleza ni miezi 36. "Kweli nyinyi mnawaacha tu? Sheria sizipo? Watu wa ardhi simpo?"


Amesema "Mkuu wa mkoa uwekezaji katika viwanja ni miezi 36 hujaendeleza nyang'anya chukua tunampa mtu mwingine".


"Na nyinyi Wakuu wa Wilaya wengine mwende mkaainishe maeneo ya fulsa za uwekezaji wa Utalii mliyonayo yaliyoshikiriwa na wawekezaji kwa miaka mingi hayana kazi yoyote wala bila kuendelezwa kwani sisi tunatangaza fulsa za uwekezaji wa Utalii miaka kumi bila uendelezwaji wowote nyang"anya kwa mujibu wa sheria maana Sheria tunazo ili tukabidhi kwa wawekezaji wengine wawekeze"

 

Mheshimiwa Mkuu wa mkoa ukiona kuna mwekezaji anamiliki kisiwa bila kuendeleza nyang'anya Sheria tunazo, watu wa ardhi mpo, hujaendeleza tunachukua tunampa mwekezaji mwingine.


"Tunatangaza fulsa, tunaita Watalii, tunaita wawekezaji halafu Kuna mtu anamiliki bila kuendeleza nyang'anya tukabidhi wengine wawekeze hayo ndio maelekezo yangu" 





No comments:

Post a Comment