Saturday, November 4, 2017

ZAO LA KOROSHO LAONGEZEKA BAGAMOYO.

 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga, akikagua godaoni la Korosho lilipo kata ya Fukayosi Halmashauri ya Bagamoyo ambapo Godaoni hili mpaka sasa limekusanya Tani 48 kutoka kwa wakulima zikisubiri siku ya mnada.
 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga amefanya ziara ya kukagua magodaoni ya korosho wilayani Bagamoyo na kubaini ongezeko la zao la korosho ukilinganisha na mwaka 2017.

Mkuu huyo wa wilaya amewataka wakulima wa korosho wilayani Bagamoyo kuzikusanya korosho zao kwenye magodaoni yaliyotengwa kwenye kila kata ili ziuzwe kwenye mnada wa serikali.

Aidha, ameonya wale wote watakaouza nje ya mnada kwamba korosho hzo zikikamatwa zitataifishwa na kuwa mali ya sehemu iliyokamata.

Alisema kuuza korosho nje ya mnada kunaipunguzia Halmashauri ruzuku ya upatikanaji wa pembejeo ambazo zinatolewa kulingana na takwimu ya mauzo ya kwenye mnada.

Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kuhakikisha hakuna walanguzi wanaokuja kununua korosho nje ya mnada ili kuiongezea korosho thamani na hataimae mkulima afaidike na kile alichokivuna.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Saidi Zikatimu aliwataka wananchi kuimarisha kilimo cha Korosho kwani ni zao ambalo linaiingizia serikali mapato na kukuza pato la mkulima kulingana na be yake kuwa juu kwa sasa.

Alisema kulingana na thamani ya korosho, Korosho kwa sasa inajulikana kama Dhahabu ya kijani hivyo kila wananchi wanapaswa kupanda miche mipya ya korosho badala ya kutegemea ile iliyopandwa zamani.

alisema agizo la serikali kila kaya inapaswa kupanda miche 30 huku kijiji kikitakiwa kupanda miche  elfu tano.

Kwa upande wao wakulima wa Korosho wilayani Bagamoyo walisema changamoto inyowakabili ni kuchelewa kwa mbolea ambapo mbolea inaletwa wakati tayari maua yameshatoka na hivyo ni vigumu kuwazuia wadudu wanaoshambulia zao hilo la korosho.
  
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga, akikagua godaoni la Korosho la kata ya Kiwangwa, kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chainze, Saidi Zikatimu wa  pili kushoto ni Diwani wa kata ya Kiwangwa, Malota husein Kwaga, mpaka sasa tani tisa zimekusanywa kijiji cha Kiwangwa.

 

Maafisa Kilimo, Ushirika, wa Halmashauri ya Chainze, wakijadili jambo wakati wa zoezi la kukagua magodaoni ya Korosho.
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chainze, Saidi Zikatimu akizungumza na wakulima wa Korosho katika kijiji cha visezi kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze wialayani Bagamoyo.


No comments:

Post a Comment