Thursday, November 16, 2017

DC BAGAMOYO ABUNI MRADI WA KILIMO KWA WATAKAOKOSA JKT.



 Waombaji wa nafasi za Jeshi la Kujenga Taifa wakiwa Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo kusubiri hatima ya maombi yao katika usaili ambao ni vijana 65 tu ndio wanaohitajika.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, Majid Mwanga, akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa usaili kwa vijana walio omba nafasi za JKT. wilayani humo.
 ..............................................
Vijana wilayani bagamoyo wametakiwa kujenga tabia ya kujitolea katika shughuli mbalimbali za kijamii ili kujenga uzalendo na nchi huku wakitarajiwa kuwa wao ndio viongozi wa baadae.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga alipokuwa akizungumza na vijana walio omba nafasi za kujiunga JKT mwaka 2017 katika usaili uliofanyika ofisi za Mkuu wa wilaya hiyo.

Alisema wilaya ya Bagamoyo imepewa nafasi 65 tu huku waombaji wakiwa 1,175 idadi kubwa ukilinganisha na miaka iliyopita.

Aliongeza kwa kusema kuwa kutokana na idadi hiyo kuwa kubwa ni wazi kuwa vvijana wengi watakosa nafasi hizo na kuwataka kubaki tabia hizo za kujitolea kama ambavyo wangeingia JKT.

Akizungumzia fursa zinazoweza kupatikana katika kujitolea ni pamoja na kuanzisha kilimo cha Muhogo na Mpunga kitakachowashirikisha vijana wote waliokosa nafasi za JKT wilayani Bagamoyo ili kuzalisha Muhogo na Mpunga na hatimae kuuza kuwa ni njia ya kujiongezea kipato kutokana na mazao hayo ya kilimo.

Alisema mpango huo utaanza mara moja na kwamba tayari heka 50 za kulima muhogo na heka 50 za kulima mpunga zimepatikana wilayani Bagamoyo lengo likiwa ni kujenga tabia ya kujitolea na kuwawezesha vijana kuwa na uwezo wa kubuni miradi itakayowasadia kujipatia kipato na kuongeza kuwa hiyo ni moja ya ajira.

Akizungumzia zao la muhogo alisema muhogo unahitajika sana nchini Oman na kwamba kutokana na mahusiano mema yaliyopo kati ya oman na Tanzania fursa ya kupeleka muhogo nchini Oman ipo kinachotakiwa ni kuzalisha kwa wingi zao la muhogo.

Aidha, aliongeza kwa kusema kuwa, katika kuhakikisha mpango huo unakuwa na manufaa asilimia tano inayotengwa kwenda kwa vijana inaweza kupelekwa kwa vijana hao watakaojitolea kulima Muhogo na Mpunga ili ziasidie katika uendeshaji wa kilimo hicho.

Kwa upande wao vijana waliozungumza na bagamoyokwanza blog walisema wamejitolea kuingia JKT bila ya malipo wakitaraji kuwa kujitolea kwao kutazaa matunda kwa siku za usoni na kwamba wazo la mkuu wa wlaya kuwapeleka kwenye kilimo watakaokosa nafasi ni wazo zuri kwakuwa litawafanya waonekane ni vijana wanaoweza kujitolea na hivyo ni rahisi kupata fursa nyingine zitakazojitokeza kwa siku za usoni.

walisema wengi hushindwa kulima kutokana na changamoto za kumudu gharama za kilimo cha uhakika, pembejeo na maeneo muafaka kwa kilimo kinachokusudiwa ambapo walisema kupitia mpango huu wa Mkuu wa wilaya wanaamini changamoto hizi zitapatiwa ufumbuzi na hatimae kufanikiwa kupitia kilimo.

Walisema licha ya kilimo hicho kutajw kuwa ni cha umoja lakini kupitia mpango huo kila mmoja atapata elimu juu ya uendeshaji wa kilimo, namna ya kukabiliana na changamoto hali itakayopelekea kupata ujuzi wa kuendesha shamba hata mtu akiwa peke yake. 

No comments:

Post a Comment