Sunday, November 19, 2017

KALE LEO SANAA NETWORK CHAONYESHA UMAHIRI KATIKA KUIGIZA.



Kikundi cha sanaa za maigizo cha Kale Leo Sanaa Network  kimefanya onyesho lake la pili katika chuo cha cha sanaa Bagamoyo, kinachojulikana kwa jina la Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) na kuonyesha umahiri wake katika fani ya maigizo.

Akizungumza na bagamoyokwanza blog, Muongozaji wa kikundi cha Kale Leo Sanaa Network, Ghoche Materego alisema kikundi hicho kinajumuisha wasanii wakongwe na wa sasa wengi wao wakiwa wamepata Elimu yao Taasisi ya Sanaa Bagamoyo (TaSUBa) lengo likiwa kukuza taaluma ya sanaa na kuonyesha maisha halisi ya wanadamu katika jamii kupitia sanaa ya maigizo.

Alisema Kikundi hicho kinapenda kutoa maigizo ya kuwaenzi mashujaa katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati ili kizazi kinachokuja kisipoteze historia ya mashujaa ambao kwa namna moja wamefanya juhudi katika kupigania haki mbalimbali za kibinadamu na kujitawala.

Katika igizo liliwavuta wengi ni lile  linaloitwa Mfumo liongo, ambapo Mfumo Liongo alikuwa ni mtu mashuhuri na shujaa aliyeishi karne ya 15 katika Pwani ya Afrika Mashariki na kwamba Historia yake itaendele kukumbukwa.


No comments:

Post a Comment