Sunday, November 12, 2017

WAOMBAJI JKT WAONYWA BAGAMOYO.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Alhaj, majid Mwanga amewataka waombaji wa nafasi za kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa JKT wilayani humo,  kuacha udanganyifu wa makazi ili kutoa nafasi kwa wakazi halisi kupata nafasi hizo.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa kauli hiyo wakati wakufunga mashindano ya Mazingira Kabumbu Cup 2017 yaliyofanyika katika uwanja wa Mwanakalenge Mjini Bagamoyo.

Alisema Rais wa Jmhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John magufuli ametoa nafasi katika kila wilaya ili kila mwananchi mkazi wa wilaya husika apate nafasi hiyo hivyo si kutoka kwenye wilaya yako kuja kuomba nafasi hizo kwenye wilaya ambayo wewe sio mkazi.

Alisema katika usaili unaotarajiwa kufanyika Tarehe 15 Novemba mtu atakaebinika si mkazi wa wilaya ya Bagamoyo atakamatwa na polisi na kuwekwa mahabusu kwa kuingilia makazi ambayo si yake ili hali nafasi hizo zipo kila wilaya nchini kote.

Aidha, Mkuu huyo wa wilaya ya bagamoyo, alitumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wakazi wa wilaya ya Bagamoyo kujitokeza kuomba nafasi hizo ambazo zipo kwa iwango tofauti vya Elimu.

Alisema nafas zilizopo ni 65 tu hivyo kila kata inaweza kutoa vijana watakaojiunga na Jeshi la Kujenga Taifa.

Aliwataka wenyeviti wa vitongoji kutoa ushirikiano katika hilo ili kuhakikisha vijana watakaoingia kwenye usaili wawe ni vijana wa Bagamoyo.

No comments:

Post a Comment