Saturday, July 22, 2017

RIDHIWANI KIKWETE AHUDHURIA MASHINDANO YA NDONDO CUP.

Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Shabiki Mkubwa  wa Timu ya Kauzu Fc Bwana Chief Kauzu akiingia Uwanjani katika Mtazamo wa kipekee, wakati mbunge Ridhiwani Kikwete alipowasili uwanjani hapo Julai 20, 2017. Mashindano ya Mpira wa Miguu ya SportsXtra Ndondo Cup yaliyoandaliwa na Cloudsfm na AzamTv. 
  
Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete, kulia meza kuu akimshangilia
Shabiki Mkubwa  wa Timu ya Kauzu Fc Bwana Chief Kauzu akiingia Uwanjani katika Mtazamo wa kipekee, 
 
 Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili uwanjani.
 
Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete akigawa Zawadi kwa viongozi wa timu ya StimTosha ya Mabibo ambao ndiyo walioibuka na Ushindi wa Magoli 4-2 kwa njia ya Penalti baada ya kumaliza mchezo kwa sare ya 1-1
 Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete, akifanya Mahojiano na Mwandishi wa Azam Tv wakati wa mapumziko. Tulizungumzia mchezo kwa kipindi cha kwanza na kutoa maoni juu ya uelekeo wa mchezo.
 
 Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete, akizungumza na aliyekuwa  kapteni  na kocha wa Timu ya mpira ya Simba, Selemani Matola.
  
Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete, Baada akizungumza na Waandishi wa Habari na kuwaasa sana Vijana kutumia fursa ya Mashindano haya kujitangaza na pia kuzishawishi timu kubwa kuja kushiriki kuangalia viwango vinavyoonyeshwa. 

Aidha, alielezeaumuhimu wa  kuwekeza katika viwanja vya michezo na kudumisha ushabiki wa timu hasa kwa maeneo wanayotoka.

No comments:

Post a Comment